@jamilakasimu2: Beki wa kushoto wa timu ya taifa ya Hispania, Marc Cucurella, amezua gumzo mitandaoni baada ya kuonekana akiondoka uwanjani akiwa amebeba Kombe la Dunia kwenye mfuko wa kawaida wa plastiki. Kitendo hicho cha kushangaza kilijiri mara baada ya sherehe za ubingwa kukamilika, huku sanduku maalum na la kifahari la kubebea kombe hilo likiwa mikononi mwa ofisa wa benchi la ufundi la timu hiyo. Video na picha za tukio hilo zimesambaa kwa kasi ya ajabu kwenye mitandao ya kijamii, ambapo mashabiki wengi wamemfurahia Marc Cucurella kwa namna anavyochukulia mambo kwa wepesi bila makuu.