@selousfmtz: KAPELA: ANSGAR CUP NI DARAJA LA VIJANA KUFIKIA SOKA LA KULIPWA Mshambuliaji wa zamani wa KMC, Kagera Sugar, Ihefu na Geita Gold, Ramadhani Kapela, amesema mashindano ya Ansgar Cup ni fursa muhimu kwa vijana wenye vipaji kuonekana na kupata nafasi ya kucheza soka la ushindani. Kapela alisema kiwango cha ushindani kilichoonyeshwa na vijana katika mashindano hayo kimemvutia, akibainisha kuwa wapo wachezaji wengi wenye vipaji wanaostahili kupewa nafasi ya kuendelea na safari ya soka la kulipwa. Alisema uwepo wa viongozi na wadau wa soka katika mashindano hayo unatoa nafasi kwa vipaji kuonekana na kuibuliwa. Aidha, amewataka waandaaji kuhakikisha mashindano hayo hayaishii kuwa sehemu ya ushindani pekee, bali yawe na mfumo wa kuwafuatilia na kuwaunganisha wachezaji walioonyesha uwezo na klabu au akademi za soka ili vipaji vyao visipotee. Alisisitiza kuwa maendeleo ya soka yanahitaji uwekezaji, wadhamini na mifumo madhubuti ya kuibua vipaji badala ya kutegemea bahati. Kapela aliyasema hayo wakati akizungumza katika uzinduzi wa mashindano ya Ansgar Cup 2026 yaliyofanyika Peramiho, wilayani Songea, mkoani Ruvuma.
Selousfm Radio
Region: TZ
Monday 20 July 2026 18:57:54 GMT
Music
Download
Comments
sjkdgl3 ⚽⚽ :
big up San broo
2026-07-21 11:41:31
0
Nasri Mbanga_ :
striker la boli
2026-07-21 08:22:33
1
Gilbert Charles 84 :
Familia yangu
2026-07-21 08:33:02
1
Mo_fire :
mjomba nakujua kwenye table afai uyo
2026-07-21 06:26:38
1
Jemsi peter :
sasa kutaja timu za zamani anakujaje😂😂😂😂
2026-07-21 11:36:05
0
❤️🇹🇿Vee Truck driver🚚❤️ :
wakunyumbaaaa
2026-07-21 07:43:45
1
LIZABONI ICON 🎒🎒🎒 :
🔥🔥🔥
2026-07-21 07:11:14
0
Mo_fire :
🔥🔥🔥
2026-07-21 06:27:33
0
junior@ laurenti :
😁
2026-07-21 15:17:16
0
To see more videos from user @selousfmtz, please go to the Tikwm
homepage.