@chawamata_tv: VIDEO: Rais wa Kenya Long Distance Truck Drivers Union, Sudi Matela, amesema madereva wa malori ndio nguzo kuu ya uchumi wa taifa, akisisitiza kuwa karibu kila sekta muhimu inategemea kazi yao, hivyo serikali zinapaswa kuwapa kipaumbele zaidi. Akizungumza katika mahojiano maalum, Matela alisema huduma nyingi za msingi zisingewezekana bila madereva, akieleza kuwa usafirishaji wa dawa hospitalini, vifaa vya shule, bidhaa za viwandani na mahitaji mengine muhimu hutegemea juhudi za madereva. "Kila nchi na kila jamii inaishi kwa sababu ya huduma ya dereva. Wagonjwa wanatibiwa kwa sababu dawa zinafika kupitia madereva, watoto wanasoma kwa sababu vifaa vinafikishwa na madereva, hata Rais anafika kazini kwa sababu ya huduma za usafiri. Dereva ndiye mzalishaji na mwezeshaji mkubwa wa uchumi wa taifa," alisema Matela. Aliongeza kuwa malengo ya serikali ya kukusanya mapato hayawezi kufikiwa bila sekta ya usafirishaji kufanya kazi kwa ufanisi, kwa kuwa viwanda, biashara na huduma mbalimbali hutegemea usafirishaji wa bidhaa. Matela pia aliitaka serikali kuboresha maslahi ya madereva kwa kuongeza mishahara, kuimarisha mafunzo ya taaluma na usalama barabarani, pamoja na kuhakikisha wanapata mazingira salama ya kazi. Alisema madereva hukabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo hatari za kiafya na za kiusalama wanapokuwa safarini kwa muda mrefu, hivyo kuna umuhimu wa kuweka sera na mifumo madhubuti ya kuwalinda. "Madereva wanapaswa kulipwa vizuri, kufundishwa nidhamu na usalama barabarani, pamoja na kupewa ulinzi na huduma zinazostahili kutokana na mazingira hatarishi wanayofanyia kazi," alisisitiza Matela. #ChawamataTV #10KFollowers #Asanteni #DarEsSalaam #Tanzania #Bongo #Habari #HabariLeo #BreakingNewsTZ #TanzaniaNews #BongoUpdates #TzUpdates #TzNews #BongoMedia #MediaTanzania #OnlineTV #TrendingTZ #TanzaniaTrending #ViralTZ #TeamChawamata #SupportLocal #madeintanzania#madeintanzania #SupportLocal #madeintanzaniat #roadto100followersontwitch #madeintanzaniawith #madeintanzania🇹🇿 #viraltz
CHAWAMATA TV
Region: TZ
Wednesday 22 July 2026 07:57:31 GMT
Music
Download
Comments
user3565056340905 :
bola we mze wetu kwa uwelewa wako
2026-07-22 09:57:19
2
7903 :
nisahii rakinikwsasa serekari imeweka uchumi kwadereva
2026-07-22 13:58:32
0
Oby oby :
ifike mahali watengeneze marobot maana udereva wa sasa barabara nzima na taasisi zinazohusika na dereva wamejaa watu ambao wanahakikisha .....au bas
2026-07-22 15:07:38
0
rank :
uko sawa kabhisa
2026-07-22 15:34:01
0
Rama Adam :
dereva tz mweu tu
2026-07-22 12:12:31
0
Isaya Lodrick :
vzr
2026-07-22 11:32:34
0
Babu % DAVOO🚛🛣 :
mzee yuko poa sana 🔥🔥🔥
2026-07-22 10:44:06
0
Tonny Kasimba :
mungu akupemaisha malefuu mzee wetuu
2026-07-22 10:24:56
0
Baraka Shirima :
nikweli kabisa mzee Mungu akuzidishie nguvu ya kutusemea
2026-07-22 10:14:44
0
utonga 87 mikazoni :
nakubali
2026-07-22 08:43:31
0
herman kifyasi :
Wambie mzee wetu,,
2026-07-22 12:59:22
0
Ramsey :
tunateseka sana mpk tumechok sasakufany hii kz
2026-07-22 11:32:35
0
MH.BM 472 JK :
Sasa Kwa nn tuna zaraulika
2026-07-22 10:01:04
0
⭐️𝐑𝐨𝐚𝐝 𝐥𝐢𝐟𝐞⭐ :
kweli kabisa ila serikali yetu hawatutambui walahi
2026-07-22 10:03:22
0
Ignas Kasila :
mzee apewe ulinzi jaman kwa heshima
2026-07-22 14:51:38
0
kelvinmwinuka3 :
nikwel mzee
2026-07-22 08:39:06
0
YAO.BOY :
Tunauwa nguvu kazi kienyeji sana madereva saiv wanaona bora kwenda kulima tu maana uko njian ni shida mno 😳😳
2026-07-22 16:44:37
0
DAGHESHY🦺 :
@am young-kotha003🤪🤪 @@ƊIĈƘ_👑 @
2026-07-22 11:50:46
2
mpangwa :
👏👏👏
2026-07-22 08:31:57
0
To see more videos from user @chawamata_tv, please go to the Tikwm
homepage.