UFAHAMU ULIMWENGU WA GIZA :
Kuna vigezo na uwezo, uwezo hua ndani ya hatima yako uliowekewa na aliekuumba. Hupati kazi, ndoa, mtoto, fedha, nyumba, gari na kadhalika simply because vigezo unavyo ila uwezo huna.
Huna uwezo kwasabbu umeibiwa hatima ambayo hubeba to be good at something tena sio good tu ni bestest than nobody.
Tutarudi palepale kwenye upishi wa pilau, mtakua watano, mtapewa mahitaji sale ya pilau nyama, lakini kuna pilau moja litakua tamu kupita zote na kutakua kuna la pili na la mwisho. Ukiniuliza kwanini nitakuambia mahitaji ya kuolewa, kuzaa, kazi, fedha, gari, nyumba na afya havitoshi kukufanya upate vitu hivyo, je nini kinatakiwa kinachotakiwa ni uwezo aliepika pilau namba moja kwa utamu maana yake ana uwezo yani hajaibiwa hatima yake hata kama hatima sio upishi ila ipo na hatima ni unstoppable wala untouchable na dynamic.
Kuna mtu hajasoma ila anakuzidi uwezo, na kuna mwanamke ana sura mbaya ila ameolewa na kuna mjinga mjinga ila ana nyumba, fedha na kila kitu ambacho wewe huna, ukiniuliza kwann nitakuambia huyo ameidhibiti hatima yake dhidi ya majangili.
Badala uwe na vigezo we kua na maarifa ya kujua je hatima na nyota bado unazo? Kama huna pigana vita urudishe kwanza na hata ukimjua adui usimuue kwa hasira utaharibu mpige arudishe kwanza bidhaa zako kisha muue ingawa waweza muacha ili umuoneshe ujeuri utakua unajimwaya mwaya na mafanikio.
Kuna wewe mwanaume umesoma lakini kuna mwanamke hajasoma ila amekushinda uwezo, mwanamke huyo anaongea kwa ujasiri, na anachapa kazi, hasahau sahau vitu, anajua nini maana ya kazi.... Na kama hamjui huyu atapemdwa na kampuni ingawa hajasoma kuliko wewe mwanaume uliesoma ila mbele ya watu unababaika(vigezov/s uwezo).
Labda niwaambie ukweli, makampuni hayataki vyeti bali yanataka uwezo, ukipiga tathimini utagundua kua kwenye magesti, lodge, ofisi za serikali kubwa mwanzo ulikua unakuta wadada warembo, lakini sikuhizi unawakuta wabibi, au wamama wabaya ndio receptionist na hawatolewagi,waenda gesti mnajua ninachosema.Imekua hivi kwasabb wale walembo hawanaga uwezo ila wana mvuto na kinachotakiwa sio mvuto bali uwezo ulioko ndani ya hatima, lakini pia mteja hahitaji mvuto tu bali uwezo na unaweza ukawa na mvuto ila uwezo huna bas
2026-07-25 18:47:38