@langgeng.pancing: Reel pancing mini, Ogawa liliput size 1000, body metal. #mancing #pancing #fishing #fyppp #foryou

Langgeng Pancing
Langgeng Pancing
Open In TikTok:
Region: ID
Monday 27 July 2026 07:40:32 GMT
332
3
0
1

Music

Download

Comments

There are no more comments for this video.
To see more videos from user @langgeng.pancing, please go to the Tikwm homepage.

Other Videos

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetangaza kuanza rasmi matumizi ya kamera za kisasa zenye mfumo wa rada na CCTV (Speed and Radar) kwa ajili ya kunasa makosa ya barabarani kuanzia Agosti 1, 2026, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha usalama barabarani na kupunguza ajali. Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Kisauni, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Dkt. Khalid Salum Muhammed amesema serikali imeendelea kuimarisha miundombinu ya barabara pamoja na kuweka mazingira rafiki yatakayosaidia kupunguza ajali zinazotokana na uzembe wa watumiaji wa barabara. Amesema ajali za barabarani zimeendelea kuwa janga nchini kutokana na baadhi ya madereva kutofuata sheria na taratibu za usalama barabarani hivyo matumizi ya teknolojia hiyo yataongeza ufanisi katika usimamizi wa sheria. Kwa mujibu wa Waziri huyo kamera hizo zitakuwa na uwezo wa kubaini makosa mbalimbali ikiwemo kuendesha gari kwa mwendo kasi kutovaa kofia ngumu kwa waendesha pikipiki kubeba abiria zaidi ya mmoja kwenye pikipiki kuendesha bila leseni kutopitisha gari kwenye ukaguzi wa usalama pamoja na kutokuwa na bima halali. Taarifa za makosa hayo zitatumwa moja kwa moja kwa mmiliki wa chombo kupitia taarifa zake za usajili. Dkt. Khalid amesema mfumo huo umewekwa kwa kuzingatia sheria za kitaifa na kimataifa huku majaribio yaliyofanyika kuanzia Julai 1, 2026 yakibaini wastani wa makosa 500 kwa siku. Aidha, amewataka wananchi wanaouza vyombo vya moto kuhakikisha wanahamisha umiliki kwa wakati ili kuepusha migogoro inayoweza kujitokeza kutokana na makosa yatakayorekodiwa na mfumo huo. Waziri huyo ameongeza kuwa kupitia Mamlaka ya Usafiri na Usalama Barabarani, utekelezaji wa adhabu kwa kutumia mfumo wa kamera utaanza rasmi Agosti 1, 2026.  Madereva watakaobainika kufanya makosa watatakiwa kulipa faini ndani ya siku 14, na watakaoshindwa kufanya hivyo watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria. #Shukuru_media#tiktokzanzibar🇹🇿🇹🇿 #tiktoktanzania🇹🇿 #usalamabarabarani#fypシ゚viral
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetangaza kuanza rasmi matumizi ya kamera za kisasa zenye mfumo wa rada na CCTV (Speed and Radar) kwa ajili ya kunasa makosa ya barabarani kuanzia Agosti 1, 2026, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha usalama barabarani na kupunguza ajali. Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Kisauni, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Dkt. Khalid Salum Muhammed amesema serikali imeendelea kuimarisha miundombinu ya barabara pamoja na kuweka mazingira rafiki yatakayosaidia kupunguza ajali zinazotokana na uzembe wa watumiaji wa barabara. Amesema ajali za barabarani zimeendelea kuwa janga nchini kutokana na baadhi ya madereva kutofuata sheria na taratibu za usalama barabarani hivyo matumizi ya teknolojia hiyo yataongeza ufanisi katika usimamizi wa sheria. Kwa mujibu wa Waziri huyo kamera hizo zitakuwa na uwezo wa kubaini makosa mbalimbali ikiwemo kuendesha gari kwa mwendo kasi kutovaa kofia ngumu kwa waendesha pikipiki kubeba abiria zaidi ya mmoja kwenye pikipiki kuendesha bila leseni kutopitisha gari kwenye ukaguzi wa usalama pamoja na kutokuwa na bima halali. Taarifa za makosa hayo zitatumwa moja kwa moja kwa mmiliki wa chombo kupitia taarifa zake za usajili. Dkt. Khalid amesema mfumo huo umewekwa kwa kuzingatia sheria za kitaifa na kimataifa huku majaribio yaliyofanyika kuanzia Julai 1, 2026 yakibaini wastani wa makosa 500 kwa siku. Aidha, amewataka wananchi wanaouza vyombo vya moto kuhakikisha wanahamisha umiliki kwa wakati ili kuepusha migogoro inayoweza kujitokeza kutokana na makosa yatakayorekodiwa na mfumo huo. Waziri huyo ameongeza kuwa kupitia Mamlaka ya Usafiri na Usalama Barabarani, utekelezaji wa adhabu kwa kutumia mfumo wa kamera utaanza rasmi Agosti 1, 2026. Madereva watakaobainika kufanya makosa watatakiwa kulipa faini ndani ya siku 14, na watakaoshindwa kufanya hivyo watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria. #Shukuru_media#tiktokzanzibar🇹🇿🇹🇿 #tiktoktanzania🇹🇿 #usalamabarabarani#fypシ゚viral

About