@licado.page: Mkoa wa Tanga umetajwa kuwa miongoni mwa mikoa inayoongoza nchini kwa idadi kubwa ya wagonjwa wa homa ya ini (Hepatitis). Akizungumza leo Julai 28 katika Maadhimisho ya Siku ya Homa ya Ini Duniani, Dkt. Penina Sikira kutoka Hospitali ya Siha Polyclinic amewataka wananchi kujitokeza kupima afya zao mapema, kupata chanjo pale inapohitajika na kuzingatia njia za kujikinga ili kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo. Afya ni mtaji. Pima mapema, linda maisha yako na ya familia yako. #licadoupdats #tangatanzania