@playstation_storetz: 🎮 SONY YATAJWA KUTENGENEZA CONTROLLER ZA KUGUSWA KAMILI Kampuni ya Sony inatajwa kuwa inafanyia kazi teknolojia mpya ya controller za PlayStation ambazo zinaweza kudhibitiwa kwa kutouch moja kwa moja badala ya kutumiabutton za kawaida. Kwa mujibu wa taarifa zinazozunguka mtandaoni, controller hizi zinaweza kutumia touchscreen au eneo kubwa la kutouch, hivyo kuruhusu wachezaji kufanya vitendo mbalimbali kwa kugusa, kupangusa (swipe) au kubonyeza sehemu tofauti za controller. Lengo ni kuongeza ubunifu katika uchezaji na kuwapa watumiaji uzoefu mpya wa michezo. Hata hivyo, ni muhimu kufahamu kuwa hadi sasa Sony haijatangaza rasmi kuwa controller hizi zitaingia sokoni. Kinachoonekana ni hati za ubunifu (patents) na dhana (concepts) zinazoonyesha mwelekeo ambao kampuni inaweza kuufuata siku zijazo. Iwapo teknolojia hii itazinduliwa, inaweza kubadilisha jinsi wachezaji wanavyocheza michezo ya PlayStation kwa kuondoa baadhi ya button vya kawaida na kuongeza njia mpya za kucheza games Je, wewe ungependa kutumia controller ya touchscreen, au unaona controller za sasa zenye button bado ndizo bora? 👇🎮 . . . . . #tanzania #fyp #tanzaniatiktok #simbasc #yangasc