@uhondo.tv: Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amesema hakuna kanuni mpya kuhusu usajili wa wachezaji 40, bali ni msisitizo wa kanuni iliyopo tangu kipindi cha UVIKO-19 (COVID-19). Akizungumza na waandishi wa habari leo, Karia amesema baadhi ya watu hawajasoma vizuri kanuni hiyo, akieleza kuwa ilianzishwa wakati wa COVID-19 sambamba na ongezeko la idadi ya mabadiliko ya wachezaji (substitutions). Amesema kwa kuwa msimu ujao ligi itakuwa na ushindani mkubwa na ratiba yenye kubana zaidi, TFF imesisitiza klabu zisajili wachezaji 40 wenye ubora, badala ya kusajili idadi hiyo kwa kujaza nafasi tu. #UhondoMICHEZONI