@.vudee: Sheikh Lema ahukumiwa kunyongwa☝️ Ajumuishwa na Mashekh wengine watano Ameandika...Bakari Mwakangwale SHEIKH Jafari Lema ambaye alikuwa Imam wa Masjid Quba Jijini Arusha, na wenzake watano, wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa na Mahakama ya Rufaa Arusha. Mahakama imetoa hukumu hiyo Jumatatu ya Julai 27, 2026, baada ya kutupa rufaa yao waliyokata Januari 2024. Hukumu hiyo wamesomewa (online) wakiwa mahabusu katika gereza la Kisonge Jijini Arusha, mbali na Sheikh Lema, wengine ni Sheikh Abashari Hassan, Sheikh Yusuph Ally, Sheikh Ramadhan Hamadi, Sheikh Abdulhasan Juma pamoja na Sheikh Kassim Idrisa. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shura ya Maimamu, Msheikh hao walikamatwa na kukaa gerezani kwa miaka tisa. Ambapo Desemba 9, 2023, Masheikh hao walihukumiwa kunyongwa mpaka kufa. Baada ya hukumu hiyo, Shura ya Maimamu Tanzania, kwa kushirikiana na familia za Masheikh hao, Januari 2024, walikata rufaa, katika Mahakama ya Rufaa Kanda ya Arusha. “Hata hivyo Julai 27, 2026, Mahakama hiyo ya Rufaa Kanda ya Arusha, imetupa rufaa hiyo na kukazia hukumu ya kunyongwa mpaka kufa. “Masheikh hao wanaungana na Masheikh wengine 14, walio hukumiwa kunyongwa, ambao wapo katika magereza ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara. Imesema taarifa hiyo. Masheikh hao sita mwaka 2014, walikamatwa na kupewa kesi ya kulipua mabomu katika mkutano wa Kanisa Arusha. Copied & Pasted from Gazeti An-Nuur #SufianMzimbiri
Vudee
Region: TZ
Saturday 01 August 2026 11:37:09 GMT
Music
Download
Comments
mudson tenga :
subhanallah awesamehe mashegh wetu
2026-08-02 18:05:01
1
mwantumu Rashid :
jamani wote tutakufa msiukumu hukumu ya mwenyezmungu
2026-08-01 14:37:00
13
mkande :
tanzania kwakuchukia mashekh inachukua nafasi yakwanza
2026-08-01 19:55:20
15
Kicwa :
ALLAH Awaokoe na hukmu hiiyo, kwani yeye ndie Mjuzi wa yasiri na dhahiri pia yeye ndie HAKIMU wa AMAHAKIMU
2026-08-02 09:05:18
5
two patna :
allah awaingiz jannatu firdausi
2026-08-02 14:46:51
2
muh :
Assakheeiir inshallah Allah yupo pamoja nawale wenye kusubiri .mpka machozi yananitoka😭😭
2026-08-01 19:27:18
4
Khadija khamisi :
yarabi hili nipijokwetu waislam basi washinde Kwa jina lako yarabi na uwape jannatul firdaus watakapo tangulia
2026-08-01 15:39:39
4
Mapembe :
lkn kuna wengine waliachiliwa huru.
2026-08-01 19:05:45
1
Khatibu Bakhero :
labda kam Dunia haja iumba mwenyezimungu lakn kam Dunia ame iumba mwenyezimungu na hao wanyongaji hukmu yao ipoh mungu awa sameh san ma shekh wetu
2026-08-02 08:39:05
9
Sahal :
Bado kuna fursa ya ku file kesi ya jumping maamuzi hayonya mahakama ya rufaa kwa Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki.
2026-08-01 23:50:46
3
thaqalain :
walikuwa na kosa gan kwan jmn
2026-08-01 14:09:42
2
pacha :
Allah ndio mlipaji wa hayo
2026-08-03 19:16:04
1
shamsur💘💥😣💎💍 :
Mbona mambo yamekua mengi jamani Aya gani inafundisha mtu kunyongwa ata kama kakosa😩
2026-08-01 20:21:19
0
mussa mwalimu :
Allah yupo na wenye kusubiri inshallah Allah awanusuru juu ya mtihani wafaulu
2026-08-02 19:16:10
0
aisha soud :
Sub-hannallah
2026-08-01 14:26:50
1
Laika Bino :
innalilah wainnailah rajiun
2026-08-01 18:14:58
1
Kimu Suleiman Juma :
mbona huyu ni Sheikh Issa Ponda?
2026-08-02 03:56:42
1
Makame Faki :
Subhanallah tunaelekea wap
2026-08-01 19:33:34
2
zaituni :
subuana llahu
2026-08-01 14:34:41
1
Halima Issa :
subhannallah
2026-08-01 14:03:37
1
Mimah Gy :
Kwani alinyonga au kuua mtu vipi anahukumiwa na hukumu hio
2026-08-01 19:30:40
1
East Africa Quality chicken fa :
Mungu atawalipia Duniya tunapita tu😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭
2026-08-01 14:06:01
1
Zainabu Ally :
Allaahu akbar mbele yenu nyuma yetu mwenyezi mungu awape pepo inshaallaah
2026-08-01 19:36:01
1
Apple Maya :
Allah awasamehe makosa yao 😭
2026-08-01 18:59:59
1
Sijambo Said :
Allah wakibr
2026-08-01 11:42:50
1
To see more videos from user @.vudee, please go to the Tikwm
homepage.