@wepesitv: Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila ametangaza rasmi kujiunga na Klabu ya Young Africans (Yanga), akisema uamuzi wake umetokana na imani aliyoipata kutokana na Uongozi wa klabu hiyo. Chalamila amesema awali alikuwa na mashaka kuhusu uongozi wa Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said lakini kwa sasa ameridhishwa na namna klabu inavyoendeshwa. “Mwanzo nilikuwa na mashaka na urais wako, Injinia Hersi lakini sasa nimejiunga rasmi nikiwa naamini nipo mikononi salama, pia ujio wa Peter Shalulile ndiyo umenifanya nijiunge na Yanga,” amesema Chalamila.