@cawabemedia_: Maafisa usafirishaji wa mtandao, maarufu kama bodaboda za mtandao, wamefunga barabara katika eneo la Chuo cha Biashara (CBE) Posta, Jijini Dar es salaam, wakipinga vitendo vya Maafisa wa Jiji kuwakamata wanapoingia katikati ya Jiji kuwachukua abiria walioita usafri kupitia programu za usafirishaji. Baadhi ya Madereva hao, ambao wamedai kuwa hukamatwa mara kwa mara wanapokwenda kuwachukua abiria waliowaagiza kupitia programu za usafirishaji ambapo wameeleza kuwa baada ya kukamatwa hupelekwa katika Ofisi za Jiji huandikiwa kosa la kupaki sehemu isiyoruhusiwa (Wrong Parking) na kutozwa faini ya shilingi 70,000. “Tunalipa ada kwa kampuni za usafirishaji wa mtandao na tunafuata masharti yote ya kazi. Lakini kila tunapokwenda kumchukua abiria tunaishia kukamatwa kwa madai ya ‘Wrong Parking’. Askari wanatupeleka ofisi za Jiji na tunatakiwa kulipa shilingi 70,000. Tumechoka na hali hii. Kama hatutakiwi kufanya kazi katikati ya jiji, basi waelekezwe kampuni za usafirishaji wa mtandao zifunge huduma hizo katika eneo hilo ili tusiendelee kupata hasara,” amesema mmoja wa madereva wa teksi za mtandao.CCMillardayo
cawabemedia
Region: TZ
Wednesday 05 August 2026 11:53:02 GMT
Music
Download
Comments
Dawson :
kwenye kampeni mnapewa mafuta ya teni mnaxhangilia mitano tena 😅
2026-08-05 13:48:52
14
mirumba :
zifungiwe wanagonga watu sana waumiza watu pikipiki wauwaji
2026-08-05 15:53:04
3
🇰🇪Enock Maluli🇨🇩🇰🇪 :
TUINGIE ROAD
2026-08-05 12:07:41
2
rama gama :
kipindi cha kampeni mnadanganywa kama watoto
2026-08-05 13:26:48
6
user1496285741215 :
simlikua mnapewa bukubuku kipindi cha kampeni wariwakopesha Sasa zinaludi mturiee tuu
2026-08-05 14:55:00
3
samah_serum :
TUFWATE Sheria hakuna aliejuu ya Sheria
2026-08-05 15:00:16
1
Jackson ac spare parts :
kila mtu ataguswa kwa wakati wake alisha sema heche
2026-08-05 14:14:14
5
Lyamba :
Baba alisema tutamkumbuka 🥺🥺R. I. P ANKO MAGU🥺🥺
2026-08-05 14:15:53
2
john materu :
hatimaye
2026-08-05 14:45:56
1
zyger12 :
oya iyo kweliiii
juzi nimekamatwa mimi bolt nikapelekwa jiji iliniuma snaa asee
2026-08-05 13:40:34
2
Kelvin John :
poleni boda wezangu 😭😭
2026-08-05 14:20:28
1
user9760882513829 :
n kweli wanaonea
2026-08-05 13:26:28
3
B52(the heart healer❣️) :
mbona mapema mno mnaanza kutoa milio maafisa usafirishaji😂😂
2026-08-05 13:31:53
2
user1707672202252 :
mwenye kiti wa bodaboda yuko kimya
2026-08-05 14:57:13
1
stady :
wanazingua sana yani kitendo chakuingia dukani unakta pikipiki washaibeba ukifika kule kuitoa elf 60000 yani mpaka unaichukia nchii
2026-08-05 14:05:56
1
Karim_fighter :
hapa ndonawakubali vijana wakibongo wanauthubutu wakutetea haki yao
2026-08-05 17:51:15
0
SUNGU ENESIA :
wewe tumewachoka sana sana,,,
2026-08-05 13:13:25
1
tanzania kigamboni viwanja :
nyumba viwanja mashamba yard beach
2026-08-05 17:33:21
0
Arakeni :
zele elfu kumi za kampeni zimeisha
2026-08-05 17:39:36
0
arafati :
serikali hii inanyanyasa sana watu hao wanaokamata wanatumwa na serikali
2026-08-05 18:11:32
0
BODA BODA WA MBAGALA :
Nachoka mimi
2026-08-05 18:21:29
1
mapanda :
kwa wanetu kwa nn msilianzshe apo apo
2026-08-05 17:42:29
0
Omary Belekete :
kwerii kabsa
2026-08-05 13:18:38
1
To see more videos from user @cawabemedia_, please go to the Tikwm
homepage.