@mariamsillogodfrey10: Shalom Family Niwape kastory kidogo juzi wakati tupo kwenye huduma znz. Kuna mtu alinitumia sms na kunipa taarifa fulani inayohusu eneo ambalo Mungu ameniitia na huyo mtu sina mazoea nae hata na wala hatujawahi wasiliana zaidi ya kusalimiana tena haizidi mara 3, kitu alichoniambia kwa kweli kwa muda huo nilitakiwa kukisikia sababu kuna namna kilitakiwa nikisogeze . Ingawa alivyoniambia alikuwa kama amepanic😄 na nadhani pia alijua kitanipanikisha nikamjibu relax Mungu anachakata. Kwanini nimekwambia hivi kuna nyakati zinakuja unahitaji watu au mtu wa kukupa taarifa iwe mbaya au nzuri nakuombea Uwe na ujasiri wa kupokea sababu haijalishi itakuwa na maumivu au furaha Mungu anataka uisikie sababu hiyo taarifa inatakiwa kukuvusha. Uwe na moyo wa ujasiri. Muwe na siku njema🙏❤️ #tanzaniantiktok🇹🇿 #viraltiktok #dodoma #kenyantiktok🇰🇪ticktoktanzania🇹🇿