@mecamedia1: 🇹🇿🔥 BODABODA NA ASKARI WAZOZANA BAADA YA MGOGORO WA NAULI: JE, KIJANA ALITUMIA BUSARA KUMPIGA ASKARI? Tukio linalosambaa kwenye mitandao ya kijamii limeibua mjadala baada ya dereva wa bodaboda kudai kuwa alimbeba askari na kumzungusha katika maeneo mbalimbali aliyohitaji, lakini baadaye kukatokea mzozo kuhusu malipo ya nauli. Kwa mujibu wa maelezo ya kijana huyo yanayosikika kwenye video, alipomdai askari nauli ndipo mzozo ulipoanza. Kijana huyo anadai kuwa askari alimng’ata kidole, na ndipo yeye akampiga ngumi akisema alifanya hivyo ili askari amuachie. Tukio hilo limeibua swali kubwa kwa wananchi: Ikiwa maelezo ya kijana huyo ni sahihi, je, alitumia busara kujitetea kwa kumpiga askari, au alipaswa kutafuta njia nyingine ya kutatua tatizo hilo? Ni muhimu pia kutambua kwamba maelezo hayo ni madai ya kijana yanayosikika kwenye video, na hayatoshi peke yake kuthibitisha mazingira yote yaliyosababisha mzozo. Wewe una maoni gani? Kijana alifanya sahihi kujitetea au alikosea kumpiga askari? Bonyeza hapa ili utu follow Meca Media: Meca Media Facebook Soma zaidi: Mecamediaafrica.com ✍️ Mwandishi: Shuri M. ##Bodaboda##Askari##Tanzania##Mzozo##MitandaoYaKijamii
mecamedia1
Region: US
Sunday 09 August 2026 21:20:02 GMT
Music
Download
Comments
Benny...199 :
usiku ning'atwe na mbu mchana ning'atwe na polisi... hii nchi ngumu
2026-08-10 05:13:30
432
oketchboy :
Police wameanza kung’ata
2026-08-10 07:55:33
71
zuuh❤❤ :
hapa unawez ukakoment alaf ukapata kesi ya uhaini buree
2026-08-10 10:26:16
59
N💕 :
Mi nna like comment ata sisem kit🥺
2026-08-10 12:51:03
0
Aisha an💙🦋🦋🦋 :
kamkosea uwez kumtoa mtu kwanzia saa 10 akuzungushe alafu usimpe nauli jmn pesa ya mafuta anapata wapi na kulisha familia dah
2026-08-10 07:53:01
112
Yusuph :
Kumbe Polisi wanag’ata bodaboda
2026-08-10 04:10:37
135
uvamizi :
Hii nd tulifundiswa kweny Civics “ABUSE OF POWER”
2026-08-10 13:08:26
0
JUDITH WIG STYLIST -TZ :
Wanang'ata hawatumi bunduki Tena aiseeee wanambinu nyingi eeeeeeeeeee
2026-08-10 10:18:20
26
Abuusalman :
Kwan askari alifanya busara kumzungusha na kumg'ata kidole?
2026-08-10 07:18:53
68
felician :
🇹🇿. Huyu kijana si sahihi kufanya kwa Askari hivi, na ninaamini Serikali itachukua utaratibu.
2026-08-10 05:42:52
29
ChAzY..wA.brAnd🎶🎶 :
mamlaka yako brother co ayo kam umemkubali mwamba na me usiniache
2026-08-10 13:59:16
8
user2700800885790 :
ndy alifanya busara kumpga police cos alimtafuna
2026-08-10 07:19:45
21
Barhromeo :
wa bongo 🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿
2026-08-10 11:32:18
1
Miss Edner❤️🦋 :
It’s so weird 😥😥💔
2026-08-10 07:59:31
1
Loveness Laizer :
Wakenya awasione hiii
2026-08-10 10:49:50
7
Achiy platnumz :
dahhh!! kwani askari akipanda boda au daladala anatakiwakulipa au
2026-08-10 07:39:46
14
lauhin :
askari Hana point😏
2026-08-10 09:02:52
1
mamabear🧸🥰 :
kaongea kwa uchungu mno
2026-08-10 09:33:30
11
RATHER :
msitumie vyeo vyenu kutunyanyasa ban sisi wote binadam
2026-08-10 09:15:34
11
yussuf3090 :
Elezea habari vizuri mbona anasema alimgata kidole usiandike kiuchonganishi sema kampiga kwasa7bu alimgata kidolee
2026-08-10 00:29:29
81
sumintaomary2 :
kafanya swa asa kunasheria gani ya askari kumngata kidole raiya aliokusudia nn namtu anadai haki yake
2026-08-10 08:38:38
11
V.N.P.S THEIR FATHER :
kijana yupo saihi maana kila mmoja yupo kwenye majukumu yake ya kila siku
2026-08-09 23:03:15
72
Mamu :
duh kazin kuna kazii
2026-08-10 07:48:27
5
Vitus Mapunda :
kijana yupo sahii
2026-08-10 04:05:03
8
To see more videos from user @mecamedia1, please go to the Tikwm
homepage.