@activevoicetv: AJALI MBAYA WATANO WAPOTEZA MAISHA HAPO HAPO.. Watu wa tano wamefariki dunia baada ya Gari ya abiria aina ya Daina yenye namba za usajili (Z 965 B) kugongana uso kwa uso na Piki piki yenye Namba za usajili (Z 452 PJ) huko katika Kijiji Cha Ziwani Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Wakizungumza kwa masikitiko makubwa Mashuhudua wa ajali hio iliyotokea alfajiri ya leo huko ziwani wamesema mnamo majira aalfajiri waliona gari likivaana uso kwa uso na piki piki aina ya boxa na watu watano kupoteza maisha papo hapo. Daktari kutoka kitengo Cha Dharura katika Hospitali ya Wilaya Vitongoji Dk Nassor Mohamed Ali amethibisha kupokea miili ya watu hao ambao tayari walishafariki dunia na baada ya taratibu kukamilika , kuikabidhi miili hiyo kwa familia zao . Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba,Abdalla Hussein Mussa amesema Chanzo cha ajili hiyo kilitokana na Mwendo kasi kwa madereva hao. #activevoicetv