@uhondo.tv: Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Ally Hapi, amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kukutana na Maaskofu wa Kanisa Katoliki kupitia Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) jana Ikulu. Akizungumza na wanachama wa CCM pamoja na wananchi wa Kilosa Mjini, mkoani Morogoro, Hapi amewataka Maaskofu hao kuwaombea viongozi wa CHADEMA ili waondokane na pepo ya ukaidi na kuitikia wito wa kwenda kwenye meza ya maridhiano. Hapi amesema Rais amekuwa akitoa nafasi kwa vyama vya siasa kukutana na kujadiliana kuhusu masuala ya Taifa, lakini CHADEMA hawajaitikia wito huo. Amesema TEC imeonyesha mfano kwa kuitikia mwaliko wa Rais na kukutana naye, hivyo amewaomba Maaskofu kutumia nafasi yao kuwaombea viongozi wa CHADEMA ili nao wafunguke na kuona umuhimu wa mazungumzo. “Maaskofu TEC, waombeeni CHADEMA. Mungu awasaidie pepo ya ukaidi iwatoke, waende kwenye meza ya maridhiano,” amesema Hapi. #UhondoTVUPDATES

Uhondo TV
Uhondo TV
Open In TikTok:
Region: TZ
Tuesday 11 August 2026 14:12:00 GMT
3199
30
6
4

Music

Download

Comments

user4703441420441
alice :
Ivi maridhiano bira chadema aiwezekani
2026-08-11 15:15:42
0
user82513052616263
the man of the people :
hatuendiii,hata siku moja
2026-08-11 15:20:32
0
jupter3348
jupter :
akuna kwenda fanyeni malidhiano na hao hao
2026-08-11 15:13:29
0
shaibumohamed465
Shaibu Mohamed :
mh ushuzi m2pu nimatumizi mabaya ya muda
2026-08-11 14:52:57
0
thabity.mziray
Thabity Mziray :
soro
2026-08-11 14:18:52
0
godyyy72
Gody adventure :
vipngoz wa dini siyo wanachama wa upinzani na mwenyekiti wao ayuko jela
2026-08-11 17:56:38
0
To see more videos from user @uhondo.tv, please go to the Tikwm homepage.

Other Videos


About