@matukioonline_tv: #HABARI Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewapongeza wananchi wa Zanzibar kwa kudumisha amani na kuonesha ukomavu wa kisiasa na mshikamano wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Akizungumza na wananchi na wanaCCM katika eneo la Kisonge visiwani humo, Dkt. Samia amesema mshikamano huo ulichangia kupandisha ushindi wa 97% ambapo amedai kuwa wale wasioitakia mema wanahoji ushindi huo.