@power_media08: KAY MZIWANDA BAADA YA KUWANYOOSHA TAKATAKA WA JAY RYTTY SASA AWAGEUKIA TAKATAKA WA MO DEWJI 'WAZEE MTUKOME' Nafikiri kwa sasa wale mashabiki na wanachama wa Simba SC yenyewe na sio Jay-Rutty SC wala Mo Dewji SC na Mangungu SC watakua wanakubaliana kwa kila neno na Kay Mziwanda ambae ameamua kukemea makundi yanayoendelea kumea ndani ya timu yao. Kay Mziwanda acheki na yoyote na ameamua kujivisha mabomu na kubeba silaha nzito na nyepesi na kuingia vitani kuwasambaratisha wale mashabiki na wanachama ambao yeye anawaita ni 'machawa' na ni 'takataka' 'mashabiki njaa' wanaotaka kuipasua Simba SC vipande vipande. Bila kuvaa darubini ya kuona mbali, kwa macho tu ya nyama kwa sasa ukiangalia Simba SC unaona kuna makundi na matabaka kinzani. Kuna kundi linalomtetea Mzabuni wa Jezi Jay-Rutty na wapo wafia Mo Dewji ambao wanamuombea mabaya Mzabuni wa jezi akwame kwenye mauzo ya jezi, Irizar likiaribu wao wana furahia na wanaposti mitandaoni na kushindwa kusajiliwa Feisal wamefanya mpaka 'House Party' kusheherekea. Na kuna kikundi sio kikubwa wala sio kidogo cha Chair man hili ni kundi linaloungwa mkono na 'takataka' na 'chawa' wengi wanaotoka upande wa Mzabuni wa jezi japo wapo na 'Wafia Mo Dewji' wachache wanaoingia na kutoka ambao wao wanapush agenda ya kutaka katiba iliyofanyiwa marekebisho na kuruhusiwa na vyombo halali vya Serikali ianze kutumika. Na hawa ni wataalamu wanajua wanachokifanya na wanajua nini kitakwenda kutoa endapo Katiba mpya ikianza kutumika, wapo nondo wameshamezeshwa maneno ya kua kama Katiba iliyoboreshwa ikianza kutumika itatamka wazi wawekezaji wataanzia watatu na sio kama ilivyo sasa tajiri ni mmoja tu. Na kama akikasirika anasema lolote analojisikia na hakuna mlango wa kutokea, na kwao wanaona Yanga SC ni kama wamefanikiwa kwenye mfumo wao mana wao wanahubiri wazi wazi wawekezaji kwao wataanzia watatu sasa kwanini Simba SC wao wabakishwe kwa mtu mmoja tu? Na wanaotaka Katiba mpya ianze kazi mara moja wanaamini ikianza kazi hakutakua na bodi ya udhamini na uendeshaji ambayo wao kwa sasa wanaiona ni bodi inayorimotiwa na mtu mmoja ambaye ni Rais wao wa Heshima na kwa kiasi kikubwa wanaamini pia ni sehemu ya kumkwamisha mzabuni wa Jezi.
K Mziwanda wewe ni mwanamke wa Nguvu sana umenyooka mimi nakupenda sana kwa fact zako wewe ni mkweli naungana na wewe
2026-08-18 08:16:06
24
🥰💐baby zuu💐💐🥰🥰 :
uko fact
2026-08-18 20:43:48
0
NICE BOY :
dada ukofact
2026-08-18 19:43:48
0
ABDULLA TZ✈. :
exactly 💯.
2026-08-18 09:28:48
0
Hussein :
Sema hii video ungepost tiktok ingetrend sana😁😁
2026-08-18 12:23:15
4
April 24 🇹🇿🇵🇹 :
Yan kumbe Mo alikua anaikopa Simba na sio kutoa pesa kama mzamini
2026-08-18 08:43:03
5
MR.X :
Simba irudi kwa Wanachama kwanza kisha Mchakato wa Udhamini ufanyike..Matatizo yote ya Simba ni Mo Dewji
2026-08-18 10:24:07
2
user4723026963812 :
twendeni kwa jakaya mlisho kikwete tumwambie kilio chetu
2026-08-18 04:23:46
1
Loyce Mafuru :
watuachie Simba yetu atujawaita makelele tu Kila siku si waende wanakotak kwenda kwan Kuna mtu kawazuia au Kuna mtu amewambia lazima washabikie Simba waende tumewachoka
2026-08-18 07:55:51
4
tumain :
kweli kbs
2026-08-18 08:44:25
2
yotham jb :
Eee wachane ukweli,alafu hao wazee ndio wana wanaalibu timu yani
2026-08-18 09:26:53
1
japhetgoliama4 :
Mnakumbuka pale jangwani mlifanya nni kwaiyo mtakologana sana
2026-08-18 06:38:35
1
adelafrancis :
Wambie kabisa
2026-08-19 13:11:45
0
mohamedi.bakari.mbinga :
K MZIWANDA UNAONGEA POINT MUHIMU SANA FLUENCERS WENGI WANANJAA SANA
2026-08-18 08:03:03
1
Sang'anya Msanu :
Kwani timu yenyewe inasemaje?
2026-08-18 16:13:13
1
allyramadhani6 :
kuna muda huyu dada ni kama namwelewa ,Kwa usemaji wake ,ila washabiki wa Simba ifike mahali ,tutimizo kauli ya Simba nguvu moja .mengine ya nn?
2026-08-18 06:32:58
1
Sara jonas :
kabisa yan wana tuchosha mungu qtusaidie leo na pamba atuvushe kwa ili
2026-08-19 11:53:08
0
Ally_Nyota Decorations ✨ :
Mangungu atuachie timu yetu
2026-08-18 10:38:58
1
Ommy White Lukona :
nakuelewa sana K mziwanda mitano tena Mungu akutunze Dada yangu
2026-08-19 09:13:09
0
Hayman luckman :
kweli kbsaaa watuwaheshimianee
2026-08-19 06:20:07
0
user5016356235732 :
waambie kabisa sisi huku mitaani ndio tumechoka haswaaa tupumzisheni tuwe nguvu moja ya kweli sio ya kinafiki
2026-08-19 15:53:11
0
Fatuma Lukombe :
NI SIMBA NGUVU MOJA
2026-08-19 16:38:10
0
@samsonedward714 :
kwani simba siku hizi hamna vikao mpaka watu wanalumbana mitandaon mbona yanga hatuyasikui?
2026-08-19 08:55:45
0
Hussein :
2026-08-18 12:23:24
1
To see more videos from user @power_media08, please go to the Tikwm
homepage.