@uhondo.tv: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta ya madini, biashara, uwekezaji, miundombinu pamoja na amani na usalama. Rais Samia amesema hayo leo Agosti 18, 2026, Ikulu Ndogo Zanzibar, mara baada ya kumpokea Rais wa DRC, Félix Tshisekedi, akieleza kuwa nchi hizo mbili zina utajiri mkubwa wa rasilimali za madini na hivyo kuna fursa ya kubadilishana ujuzi na uzoefu katika uchimbaji, uongezaji thamani na masoko ya madini. Amesema katika mazungumzo yao pia wamegusia masuala ya amani na usalama, ambayo ni nguzo muhimu kwa maendeleo ya Kanda ya Afrika na dunia kwa ujumla. Aidha, Rais Samia amesema Tanzania, kama mshirika wa karibu wa DRC, iko tayari kuendelea kushirikiana na nchi hiyo katika kujenga uchumi unaowaunganisha wananchi wa mataifa hayo, kuongeza biashara na uwekezaji, kuboresha miundombinu na kujenga mazingira ya amani na ustawi wa pamoja. Kuhusu miundombinu, Rais Samia amesema kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya Kalemie–Manono kutasaidia kuunganisha Tanzania na DRC, huku ikichochea shughuli za kiuchumi katika nchi hizo mbili pamoja na ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Ameongeza kuwa Tanzania na DRC zimesisitiza umuhimu wa kuimarisha biashara kwa kuondoa vikwazo visivyo vya lazima, kuboresha huduma za mipakani na kuwezesha sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika fursa zitakazojitokeza. Rais Samia amesema ziara ya Rais Félix Tshisekedi nchini Tanzania imefungua ukurasa mpya wa kuimarisha zaidi uhusiano wa kihistoria na ushirikiano wa kimkakati kati ya Tanzania na DRC. #UhondoTVUPDATES
Uhondo TV
Region: TZ
Tuesday 18 August 2026 12:57:41 GMT
Music
Download
Comments
Myfiles Documents :
Asante
2026-08-19 06:55:27
0
Charly kiunda :
donc c'est pas nous seule que kisekedi trompe ?
2026-08-19 08:15:24
14
Mr osman nathan :
mfundishe kujenga barabara za kuonganisha mikoa huyo
2026-08-19 13:29:36
3
Elon Musk :
Tanzania na DRC sasa ni ndugu asante sana mama samiya kwaku shirikiyana nasi
2026-08-19 15:41:40
4
ktm :
il vous a promis quoi ????🤣🤣🤣🤣🤣
2026-08-19 09:29:34
2
John Sungura :
Uongo mutupu Tchisekedi anakuambia
2026-08-19 07:07:45
4
mr gain without pain. :
MADINI!!!?, DRC watusaidie kuchimba?
2026-08-18 13:22:04
3
sylver boy nyuki :
Karibu drc mama ila uchunge sana kumejaa matapeli?
2026-08-19 09:18:45
2
vanboy de bunia🗽Ⓜ️TZ :
vraiment suis ravie d'écouter ça 😅
2026-08-19 07:04:25
3
masunzu kyavwenda :
Kumbe siyo sisi pekeyake tunaye danganywa na tsisekedi
2026-08-19 12:29:32
2
ELIAS :
Hapo umenifuraisha wa Zambia wametutesa sana
2026-08-19 07:15:55
2
Yves Le Sage :
Tanzania, Burundi , CongoDRc tupo wandungu
2026-08-19 16:04:07
0
salimu :
mwambie Rais chiseked atuondolee kanyaka tumeichoka
2026-08-18 18:38:59
1
Grand Maître Yoda 😶🌫️🤞🏾 :
Attention avec lui,…
2026-08-19 11:40:11
0
volonté$$$ :
next
2026-08-19 16:09:38
0
moïse :
asate sana
2026-08-19 16:54:13
0
Donatien Omenu :
Ufanye wangalisho sana kuakuwa Raïs wetu tshisekedi haeshiyake mapatano.
2026-08-19 07:36:35
1
judith mufungizi :
shisekedi ndio nani
2026-08-19 15:59:51
0
Emmanuel bishikwabo :
waza
2026-08-19 14:31:58
0
Atibu Mao :
vraiment
2026-08-19 13:00:16
0
chrismenmenko :
asante sana mm ❤️❤️🇨🇩🇹🇿
2026-08-19 14:42:57
0
Louis+Aisha and familly :
karibu kwa muungano wako muheshimiwa mama samia suluhu Mungu akubariki
2026-08-19 15:25:34
0
chekedi siyo mm ni tshisekedi 🤣🤣
2026-08-19 13:50:36
0
kalonda Pascal :
un bon projet
2026-08-19 17:02:09
0
maestro123 :
DRC 🇨🇩 🤝TANZANIE 🇹🇿
2026-08-19 05:09:05
0
To see more videos from user @uhondo.tv, please go to the Tikwm
homepage.