@zaramoonlinetv: Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa angalizo la uwezekano wa mvua kubwa zinazoathiriwa na El Niño kuanzia wiki ya nne ya Septemba hadi Oktoba 2026, huku athari zikitarajiwa kuendelea hadi Januari 2027. 📍 Maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani ni pamoja na: 🔹 Kanda ya Ziwa Victoria 🔹 Dar es Salaam 🔹 Tanga na Pwani 🔹 Kaskazini mwa Morogoro 🔹 Zanzibar 🔹 Arusha, Manyara na Kilimanjaro TMA imesema ongezeko la mvua linatarajiwa zaidi Novemba 2026, huku mvua zikitarajiwa kuendelea hadi Januari 2027. ⚠️ Mvua hizo zinaweza kusababisha mafuriko, uharibifu wa mazao na miundombinu, unyevu kupita kiasi kwenye udongo na kuongezeka kwa magonjwa. 👨🌾 Wakulima na wadau wa sekta mbalimbali wametakiwa kujiandaa mapema, huku wananchi wakihimizwa kufuatilia taarifa rasmi za hali ya hewa kutoka TMA. 📹 ZARAMO ONLINE TV 📰 #HabariZoteZikoHapa #TMA #ElNino #Mvua #WeatherTanzania