@nuktatanzania: Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amesema yeyote anayehisi amekosea kwa kutoa agizo la mabasi yote kuanzia na kumalizia safari zake katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli ampeleke mahakamani. Akizungumza na wananchi leo Agosti 19, 2026 katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli, Mbezi, Dar es Salaam, Chalamila amesema baadhi ya watumishi wa umma wamechangia kukiua kituo hicho kwa kupokea ongo na kusisitiza kuwa yeye ni ngumu kwa mtu kummudu.