@bongofive: Wasanii mnikumbuke” — Mariam, Mke wa Mandojo Mariam, mke wa msanii Mandojo, amewaomba wasanii wenzake kumkumbuka mara kwa mara baada ya baadhi ya wasanii walioshiriki kwenye maadhimisho ya miaka 30 ya Bongo Fleva kumtembelea na kumjulia hali nyumbani kwake Iyumbu, mkoani Dodoma. Akizungumza kwa uchungu, Mariam amesema familia yake bado inahitaji msaada na kuwasihi wasanii hao kutowasahau, bali waendelee kuwafikia na kuwasaidia pale wanapoweza. Ziara hiyo imekuja ikiwa ni sehemu ya wasanii hao kuonyesha mshikamano na kumjulia hali mke wa msanii huyo. Kwa Madee na FID Q ambaye ni waratibu wa tukio la miaka 30 ya BongoFleva watakuwa na familia hiyo katika kipindi chote baada ya kutembelea hapo. Imeandaliwa na @yasiningitu