@chawamatasystem: VIDEO: Shabiki wa Simba SC ametoa maoni yake baada ya timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Singida Black Stars. Pamoja na furaha ya kupata pointi tatu, shabiki huyo amesema bado kuna jambo la msingi linalopaswa kufanyiwa kazi ndani ya kikosi. Amesema wachezaji wanapaswa kuambiwa ukweli kuhusu umuhimu wa kuwa na nidhamu wanapokuwa uwanjani. Kauli hiyo imekuja baada ya Antony Mligo kuonyeshwa kadi nyekundu katika mchezo huo. Kwa mujibu wa shabiki huyo, kupata ushindi ni jambo la kufurahisha, lakini kupoteza wachezaji kwa kadi nyekundu kunaweza kuiweka timu kwenye changamoto katika michezo inayofuata. Ameitaka Simba kuhakikisha inarekebisha suala hilo mapema. 🗣️ “Wachezaji waambiwe ukweli, nidhamu inahitajika uwanjani,” amesema shabiki huyo, huku akisisitiza kuwa Simba SC inahitaji kuwa makini zaidi ili kuendelea kupata matokeo mazuri. Credit: @m15_tv
Leo umeongea Ukwl sio kila siku ushabiki kuna kipind ukwl Usemwe,Safii sana Mvhungaji
2026-08-23 06:05:36
0
Aminata :
yes umeongea vizur man kun watu wengine wanalalamika bila kuelewa ,mchezaji anatakiwa awe na nidham muda wote
2026-08-23 05:23:40
1
lawrencendosy :
unasema kweli broo ww nishabiki kweli broo salt kwako mkuu
2026-08-23 14:49:10
0
Alex Julius :
umeongea point kabisa
2026-08-23 06:26:52
0
aloycemashaka1 :
Wanaichiii like kwaajili yahuyu jamaa ameongea poit sanaaa
2026-08-23 07:04:18
0
DASH__MITINDO :
Afu card tunapata ktk mechi ndogo zisizo na pressure….always team ndogo ndo zinapataga red mbele ya timu kubwa leo sisi ndo tumegeuka tunapata red….dahhhhhhh
2026-08-23 07:02:13
0
To see more videos from user @chawamatasystem, please go to the Tikwm
homepage.