@omarimshairi: SELEMANI MWALIMU: SIMBA NDIO WAMESHIKILIA MPINI! Suala la Selemani Mwalimu kutocheza Yanga hadi sasa linaendelea kuibua maswali mengi. 👀 Taarifa zinazoendelea kusambaa zinaeleza kuwa Simba SC hawajafungua njia kirahisi, licha ya Yanga kufanikiwa kumpata Mwalimu kutoka Wydad Casablanca kwa mkopo. Simba awali walikuwa wametangaza kuwa mshambuliaji huyo angeendelea kuwa sehemu ya kikosi chao msimu wa 2026/27. 🔥 Kwa lugha rahisi, mpira bado uko kwenye mikono ya Simba—ndiyo maana Mwalimu hajaanza kuonekana uwanjani akiwa na Yanga kama mashabiki walivyotarajia. Hii siyo ishu ya kocha kutaka au kutotaka kumtumia Mwalimu, bali inaonekana kuna jambo la kiutawala/kimkataba linalozuia ushiriki wake kwa sasa. 👀 Je, Simba wataendelea kushikilia mpini hadi mwisho, au Mwalimu ataonekana uwanjani akiwa Jangwani? #yanga #SimbaSC #selemanimwalimu🔥🔥 #simbasportsclub #NBCPremierLeague