@official_papaambalamwezi: CHANJO YA NEWCASTLE YA VIFARANGA VYA SIKU 7 NI TOFAUTI NA YA SIKU 21 UKICHANGANYA UTAKUWA HUJATOA CHANJO wengi wetu tunachanganya hizi chanjo mbili kwa sababu zote ni za Newcastle. Siku ya 7: Mara nyingi hutumika Newcastle HB1 kuanzisha kinga kwa vifaranga na sawa na Mtoto mdogo kumpa maziwa sio ugali hivyo usimpe kifaranga wa siku 7 chanjo ambayo ulitakiwa kumpa wa siku 21 Siku ya 21: Mara nyingi hutumika Newcastle LaSota kama booster ya kuimarisha kinga. Hivyo ukimpa HB1 ambayo ulitakiwa kumpa kifaranga cha siku 7 haitakuwa vizuri ni sawa na kumlisha mtu mzima anaelima uji wa mtoto Kwa hiyo, HB1 ya siku 7 na LaSota ya siku 21 si kitu kimoja kwenye ratiba ya chanjo. Usiangalie jina “Newcastle” pekee. Angalia aina ya chanjo na siku inayotakiwa kutolewa. Ukichanganya ratiba, unaweza kudhani umewapa chanjo wakati ratiba yako haijakamilika vizuri. #chanjoyanewcastle #ufugajiwakuku #vifarangavyakuku @highlight