@jvckieseven: kila mtu alitafuta namna ya kuingia mjini kiutofauti ili kuliteka soko la music bongo. ndipo alipoibuka huyu mwamba hapa wakuitwa ABEL MOTIKA (MR EBBO) na style yake ya kimaasai na alifanikiwa. huyu jamaa alikua producer wa muziki ambaye kwa asilimia 80 ya kazi zake alitengeneza mwenyewe kwenye studio yake ya motika rekodi mkoani Tanga japo nyimbo zake za awali alirekodi kwenye kikontena cha Master Jay (MJ records) mwishoni mwa mwaka 1999 kuingia 2000, na huyu jamaa ndiye msanii mwenye albam nyingi zaidi wakichuana na sugu. Bad news ni kwamba 2011 industry ya bongoflava ilipata pigo la kuondokewa na huyu mkali ambaye mpaka sasa pengo lake halijazibika kwa style ya muziki wake. R I P MR EBBO 😭😭