@vibesfm106.5_: Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemteua Deograatius John Ndejembi kushika nafasi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya nafasi hiyo kuwa wazi kufuatia kujiuzulu na kisha kufukuzwa uanachama kwa aliyekuwa Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi. Jina la Ndejembi sasa linatarajiwa kuwasilishwa Bungeni kwa ajili ya kupigiwa kura, na endapo litapitishwa atakuwa Makamu wa Rais Mteule baada ya Dk Nchimbi ambaye alijiuzulu hapo jana.