@leodigital5: MWANAMKE WA MIAKA 39 AZUA MJADALA BAADA YA KUTANGAZA KUWA BIKIRA Mwanamke mwenye umri wa miaka 39 kutoka Maple Falls ameibua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kutangaza hadharani kuwa anajivunia kuwa bikira na kwamba hana mpango wa kubadili uamuzi huo katika maisha yake. Crystal Evergreen amesema alifanya uamuzi huo kwa hiari yake miaka mingi iliyopita na hajawahi kuhisi kushinikizwa kuubadilisha, licha ya kuishi katika jamii ambako mahusiano ya kimapenzi ni jambo la kawaida. Amesema anataka msimamo wake uwe mfano kwa watoto wake, akisisitiza umuhimu wa kufanya maamuzi binafsi bila kufuata shinikizo la jamii au kile kinachofanywa na wengine. Kauli yake imezua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii. Baadhi ya watu wamemsifu kwa kusimamia uamuzi wake, huku wengine wakisema thamani ya mtu haiwezi kupimwa kwa historia yake ya kimapenzi pekee. Wakati mjadala ukiendelea, maelfu ya watu wameendelea kutoa maoni tofauti kuhusu uamuzi wake, huku wengine wakisisitiza kwamba masuala ya maisha binafsi yanapaswa kuheshimiwa. WEWE UNAONAJI MSIMAMO WAKE?