@rashid_mansa: RWANDA IMEWAKA! DIAMOND PLATNUMZ AMEITIKISA KIGALI! Ripoti kutoka kwa waandaaji wa show ya Diamond Platnumz huko Rwanda leo zinadai kuwa ukumbi umetapika watu, huku mashabiki wakijaa kila kona kiasi kwamba hakuna pa kukanyaga! Inasemekana ukiamua kutoka nje kwenda kupata hewa kidogo, ukirudi unaweza usipate tena nafasi ya kukaa! Wakazi wa Kigali na viunga vyake wamejitokeza kwa wingi kumshuhudia Mfalme wa Muziki kutoka Tanzania akilitawala jukwaa. Na hii si mara ya kwanza kwa Diamond kufanya show Rwanda. Msanii huyo ameshawahi kutumbuiza nchini humo mara kadhaa, na kwa namna mashabiki wa Rwanda wanavyompokea kila anaporudi, Rwanda sasa imeanza kuonekana kama nyumbani kwake! Diamond Platnumz akifika Rwanda, mashabiki wanajua kazi yao. Wasafi wamevuka mipaka! #diamondplatnumz #rwandatiktok🇷🇼🇷🇼 #tiktoktanzania🇹🇿🇹🇿 #tiktokzambia🇿🇲🇿🇲 #kenyantiktok🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪