@chawamatasystem: VIDEO: Timu hizo mbili zina wachezaji wanaovutia si kwa uwezo wao wa kucheza soka pekee, bali pia kwa kuonyesha uwezo wa kucheza muziki na kuleta burudani nje ya uwanja. Kwa upande wa Simba SC, Neo Maema amekuwa miongoni mwa wachezaji wanaoonyesha uwezo huo, huku Yanga SC ikiwa na Mohammed Hussein na Clement Mzize. Swali: Kati ya Neo Maema, Mohammed Hussein na Clement Mzize, nani anaonekana kuwa “dansa” bora zaidi linapokuja suala la kucheza muziki? 😂🎶