@abdrash_: Kushukuru ni sifa ya waumini.. 1. Muumini anaona Neema nyuma ya Neema. Asiyemuaamini anaona "nilijitahidi mwenyewe". Muumini anasema "Alhamdulillah, Allah kanijalia". Anaona mkono wa Allah hata kwenye vitu vidogo. 2. Kushukuru kunazidisha. Allah mwenyewe ametuahidi: “Mkinishukuru, nitakuzidishieni” [14:7] Shida ikija muumini anashukuru kwa subira. Neema ikija anashukuru kwa sifa. Hivyo anashinda pande zote mbili. 3. Kutoshukuru ni sifa ya Iblisi. Iblisi alisema: "Na hutasikia wengi wao wakishukuru" [7:17] Kwa hiyo mtu asiyeshukuru anatembea na tabia ya shetani bila kujua. Namna za kushukuru kama waumini: 1. Kwa moyo - Tambua ndani kwamba ni kutoka kwa Allah. 2. Kwa ulimi - Sema "Alhamdulillah" mara nyingi. Hata kwa kitu kidogo. 3. Kwa vitendo - Tumia neema hiyo kumtii Allah. Mtume ﷺ alisimama usiku mpaka miguu yake ilivimba. Aulizwa "Mbona ewe Mtume, wakati Allah amekusamehe dhambi zako?" Akasema: "Je, nisiwe mja mshukuru?" Angalia.. Alikuwa na kila kitu. Lakini Bado Alishukuru. Ukumbusho Leo: Muumini anajua: Kila kitu ni kutoka kwa Allah. Na kila kitu kina hekima.