@fredmsungu: MAISHA NA UTUMISHI- Part 1 Mathayo 6:24, Yesu anafungua code kubwa kuhusu uhalisia wa maisha na dhana ya mafanikio makubwa. Kitu kikubwa kinaonekana hapa… maisha yamefungamanishwa moja kwa moja na utumishi. Na kiwango cha mtu cha utumishi (service) kwenye upande aliopo ndiyo kinaamua kiwango cha mafanikio yake. Ambayo kimsingi kwenye ulimwengu wa roho ni uwezesho tu kwa ajili ya kutumikia kusudi unalotumikia. Kweli hii ukiielewa itaanza kukupa kutafakari kwa kina sana juu maana ya maisha.