@jwtz80: Sehemu ya KWANZA. ~~~~~~~~~~~~~~~~ Tunaanza kudodosa kwata, doso na mapigo na mwendo ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), mwaka 2024 wakati JW inatimiza Miaka 60 tangu kuanzishwa kwake, Kurugenzi ya Habari na Uhusiano ya Jeshi iliaandaa makala mbalimbali kumulika miongo sita ya jasho, nguvu, ujuzi na safari nzima ya chombo hicho muhimu kwa ulinzi wa taifa. Miongoni mwa makala hayo ni kuhusu Kamandi Sita za JWTZ. 1. Kamandi ya Jeshi la Wanamaji 2. Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu 3. Kamandi ya Jeshi la Anga 4. Jeshi la Kujenga Taifa 5. Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi 6. Kamandi ya Jeshi la Akiba Tuanze kuzifahamu aste aste walau kwa uchache! KAMANDI YA JESHI LA NCHI KAVU, inafungua lango la maarifa haya adhimu na adimu.