@jambotv_: VIDEO: Baada ya mapumziko mafupi mchana wa leo, kesi ya uhaini namba 19605/2025 inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Antiphas Lissu, ilirejea huku Katibu Mkuu wa chama hicho, John John Mnyika, akipanda kizimbani kukabiliana na maswali ya dodoso kutoka kwa Wakili wa Serikali Mkuu, Nassor Katuga. Moja ya maeneo yaliyozua mjadala ni pale Katuga alipohoji kama raia yeyote, ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti wa CHADEMA, ana haki ya kuzuia uchaguzi mkuu uliowekwa kwa mujibu wa Katiba ya nchi. Mnyika alitoa jibu akisema, "Ni haki kwa uchaguzi usio huru na wa haki, ni haki kuuzuia kwa njia za kidemokrasia. Ni haki kabisa". Amesisitiza kuwa wananchi wana haki ya kushiriki uchaguzi ukiwa huru, wa haki na halali tu. Katuga alimtaka Mnyika kufafanua kile alichokisikia wakati wa hotuba ya Tundu Lissu katika mkutano wa watia nia wa Aprili 3, 2025. Mnyika alikiri kusikia kauli za ‘Polisi kukimbia na mabegi ya kura’, ‘tunaenda kuzuia uchaguzi’ na ‘tunaenda kukinukisha’ akisema kuwa Lissu alifafanua kauli hizo. Katuga alipohoji kama Mnyika ameleta mahakamani hotuba hiyo inayofafanua maneno hayo, Mnyika alijibu: "Nimeileta kwa maelezo ya mdomo kwasababu si wajibu wangu kuthibitisha mashtaka". Katuga alijaribu kumjenga Mnyika kama shahidi mwenye masilahi binafsi (interested witness) katika kesi hiyo, kwa kuwa uteuzi wake kama Katibu Mkuu ulipendekezwa na mshitakiwa (Tundu Lissu), na kwamba yeye ndiye aliyeratibu kikao cha Kamati Kuu cha tarehe 29 Agosti 2026 kilichoazimia kumtetea Lissu kwa nguvu zote. Mnyika alikataa vikali madai hayo akieleza kuwa masilahi yake katika kesi hiyo yanawakilisha masilahi ya chama (party interest) na masilahi ya umma (public interest), na siyo masilahi yake binafsi.

Jambo TV
Jambo TV
Open In TikTok:
Region: EN
Monday 31 August 2026 18:44:36 GMT
76652
2637
25
64

Music

Download

Comments

cest.le.fraitel
c'est Le Fraitel :
very clean response
2026-09-01 17:30:33
0
user290509140
Simon :
mungu simamia kesi ya lissu
2026-08-31 23:52:27
6
my17630
My1 :
Mstakiwa ni Mwansheria, shahidi ni mwanasheria. kazi kweli kweli
2026-09-01 13:44:10
0
pattiepatrice
pattiepatrice :
masilahii kwnn mtahabixhe mwenzenu hvo
2026-09-01 13:34:11
0
user18341719390250
user18341719390250 :
chadema wote ni wanashelia
2026-09-01 12:44:01
1
user3668521796162
furaha :
Mungu simama na mashahidi wa Lisu
2026-09-01 14:30:28
0
user039638891
Freeman :
2026-09-01 14:35:47
0
user81035695116692
PELEGORE 🤔🤔🤔🤔 :
Nakubali
2026-09-01 17:52:46
0
forgohzcmlg
Dorcas :
2026-09-01 09:38:02
0
user2257160044398
kamwana :
Nawaombeeni wa Tanzania mpate katiba mpya itakayo tambua haki za wa' Tanzania. Mungu mbele ndugu zetu waTanzania🫶
2026-09-01 12:33:21
0
user53420233585950
user53420233585950 :
Pamoja Mungu awstetee
2026-08-31 20:33:34
1
mpendahaki3
mpenda haki :
Amina mnyika
2026-08-31 20:17:38
0
engineer_senator
Eng Senator :
Mungu atasimama pamoja nanyi
2026-09-01 04:33:50
0
abdallah.kibeku
Abdallah Kibeku :
chizzzz
2026-09-01 19:11:47
0
robertkatemi3
Katemi :
tutashinda kwa kishindo, dhuruma ina mwisho wake
2026-09-01 10:44:34
0
masunzufurniture
Masunzu Furniture :
nikweli mnyika hana masilahi na lisu
2026-09-01 04:35:56
0
user47266941046922
user47266941046922 :
Raha ya viongozi wa chadema ni vichwa kweli kweli. Ushindi kwao ni mkubwa! Mungu yu pamoja nanyi.
2026-09-01 15:08:35
0
kain.mtuluwa
Kain Mtuluwa :
kumbe munyika nae Yuko vizuli sana
2026-09-01 20:16:38
0
georgenjaromollel0
George Njaro Mollel :
😁😁😁
2026-08-31 19:47:50
0
bahati.windo8
Bahati Windo :
💪💪💪
2026-08-31 21:06:16
0
fanujrsn6nu
Bill :
😳😳😳
2026-09-01 19:25:07
0
To see more videos from user @jambotv_, please go to the Tikwm homepage.

Other Videos


About