@millardayo_: Klabu ya Yanga imemtumia Mwandishi nguli wa Habari za Michezo duniani, hususan masuala ya usajili, Fabrizio Romano raia wa Italia, kutambulisha jezi zake za Kimataifa zitakazotumika katika michuano ya CAF Champions League msimu wa 2026/2027. Romano, ambaye amejizolea umaarufu mkubwa duniani kupitia habari za usajili wa Wachezaji na kauli yake maarufu ya "Here We Go", ametumika katika utambulisho huo ikiwa ni sehemu ya Yanga kuongeza ukubwa wa chapa yake Kimataifa. Yanga inaiwakilisha Tanzania katika CAF Champions League msimu huu ikiwa na dhamira ya kufanya vizuri zaidi katika michuano hiyo ya Afrika. #MillardAyoUPDATES