@gerver.pharmacy.t: Ovulation ni pale ambapo yai lililokomaa linatoka kwenye ovari na kuwa tayari kurutubishwa. Sasa kuna dawa ambazo hutumika kuchochea ovulation, mfano Clomiphene. Tatizo ni kwamba, baadhi ya wanawake wanatumia dawa hizi kwa lengo la kupata mimba bila kwanza kujua kama kweli tatizo lao ni kutoku-ovulate. Na hapa ndipo tunahitaji kuwa makini. Kwa sababu kuchochea ovulation ni kusaidia hatua moja tu katika mchakato wa kupata ujauzito. Haimaanishi kwamba mimba itapatikana moja kwa moja. Kwa hiyo, usitumie dawa ya kuchochea ovulation kwa sababu tu umeambiwa “hii ni dawa ya kupata mtoto.” Kwanza jua inafanya nini, umepewa kwa sababu gani, na kama kweli inakufaa. Pharm. Oliver #pharmacytiktok #viraltiktok #ujauzito #pharmacist