@bashasha_tv: DODOMA:Mama mmoja na mtoto wake mwenye umri wa miaka mitatu wamefariki dunia baada ya kujeruhiwa katika ajali ya moto iliyotokea jana jioni, Septemba 3, 2026, katika Kata ya Kizota, Jijini Dodoma. Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Diwani wa Kata ya Kizota, Jamal Ngalya, amesema chanzo cha moto huo kinadaiwa kuwa ni hitilafu ya umeme iliyotokea katika eneo la fundi wa uchomeleaji (welding). Kwa mujibu wa Ngalya, mama huyo pamoja na mtoto wake walijeruhiwa katika tukio hilo na kukimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya matibabu, lakini baadaye walifariki dunia wakiwa hospitalini. Kwa upande wake, Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Dodoma, Mrakibu (SF) Rehema Menda, amewashukuru na kuwapongeza wananchi wa Kizota kwa kuwa watulivu na kushirikiana na Jeshi hilo wakati wa zoezi la uokoaji na uzimaji wa moto. Menda amesema ushirikiano wa wananchi ulikuwa muhimu katika kuwezesha shughuli za uokoaji na udhibiti wa moto kufanyika kwa ufanisi. #bashashatvupdates #bashashadigital #bashashamedia
bashasha_tv
Region: TZ
Friday 04 September 2026 06:38:22 GMT
Music
Download
Comments
miss Zahara 😘🥰 :
duuuh jamn kizota jamn 😭😭😭
2026-09-04 13:01:01
0
rey qeen💞💞💞 :
Nachukia kuckia Au kuona mtu wa Dodoma akipata shida Mungu nilindie mkoa wangu 🥺🥺🥺🥺🥺🥺
2026-09-04 08:13:16
17
1212 :
poleni
2026-09-04 11:24:27
0
ney cute baby 🤩🤩 :
daah hii ajali tumeipita jana kizota maskini😭😭
2026-09-04 09:53:37
1
🌹♥️dayana💕❤️ :
mmh ni wapi kipenziii
2026-09-04 07:47:27
0
dismasprivatus :
daaah pumzika kwa aman🥺🥺
2026-09-04 08:18:51
2
Aisha yahaya 🥰🥰 :
nijilan yangu jaman
2026-09-04 15:53:22
0
Elizabeth fransic :
𝕁𝕒𝕞𝕒𝕟𝕚 𝕞𝕟𝕘𝕦 𝕒𝕨𝕒𝕡𝕠𝕞𝕫𝕚𝕤𝕙𝕖
2026-09-04 17:28:30
0
vassy cute... :
Daah🙏
2026-09-04 15:51:43
0
🖇️Isha🥰🥰 :
Jamani daaa
2026-09-04 08:24:31
0
tiner💞💜😍 :
daah!! yani roho imeniuma sana mama na uyo mtoto jana jaman kizota😢😢
2026-09-04 13:19:31
0
Nemah :
🙆😭😭
2026-09-04 07:59:58
0
grace :
mwenyezi MUNGU azilaze roho za marehemu mahali pema peponi😭😭😭😭😭😭😭 inauma sana poleni
2026-09-04 06:57:14
0
@ Allyjuma123 :
daah poleni sana wafiwa na Mungu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu
2026-09-04 07:37:53
0
DALALI_MROSSSO_DODOMA :
tumia lugha nzur ni tanesco so maneno
2026-09-04 08:51:41
0
To see more videos from user @bashasha_tv, please go to the Tikwm
homepage.