@joseph_yona_: Dkt. Khamis Mussa, mchambuzi wa masuala ya siasa, amemtaja Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba kuwa ni “tatizo kuu la matatizo ya Watanzania”, akidai kuwa sehemu kubwa ya changamoto zinazohusu Katiba nchini zinatokana na nafasi na maamuzi ya Warioba katika vipindi mbalimbali vya historia ya Tanzania. Akizungumza leo Ijumaa, Septemba 4, 2026, Dkt. Mussa amesema Warioba ndiye aliyeandika Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, akidai kuwa Katiba hiyo ilimpa Rais madaraka makubwa kiasi kwamba hata Mwalimu Julius Nyerere alilazimika kuifanyia marekebisho mwaka 1982 na 1984. Amesema kinachomshangaza ni baadhi ya wakosoaji wa Katiba hiyo kumtaja Warioba kama shujaa licha ya kuwa ndiye aliyeshiriki kuiandaa. Dkt. Mussa pia amemlaumu Warioba kwa kile alichokiita kushindwa kutumia nafasi aliyopewa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete kupitia Tume ya Mabadiliko ya Katiba, akidai kuwa mapendekezo ya Serikali Tatu yaliyotokana na Tume hiyo ndiyo yaliyoibua mvutano mkubwa katika Bunge Maalum la Katiba mwaka 2014 na hatimaye kuzuia kupatikana kwa Katiba Mpya. Kwa mujibu wa Dkt. Mussa, kama pendekezo hilo lisingekuwepo, huenda Tanzania ingekuwa tayari imepata Katiba Mpya. Akizungumzia mwenendo wa Warioba baada ya kustaafu, Dkt. Mussa amesema tofauti na viongozi wastaafu kama Cleopa Msuya na Benjamin Mkapa ambao, kwa mujibu wake, walikuwa wakitoa ushauri kwa viongozi walioko madarakani moja kwa moja, Warioba amekuwa akizungumza kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii. Amehusisha kauli za Warioba kuhusu matukio ya Oktoba 29, 2025 na madai ya mgawanyiko ndani ya Jeshi la Polisi na kusema kuwa kiongozi mwenye uzoefu kama Warioba alipaswa kutumia nafasi yake kumshauri Rais moja kwa moja badala ya kulalamika hadharani. Dkt. Mussa amemkosoa zaidi Warioba kwa kutumia taarifa zilizokuwa zikisambaa mitandaoni kuhusu idadi ya vifo vilivyotokana na matukio ya Oktoba 29, 2025, akisema taarifa rasmi kuhusu idadi hiyo haikuwa imetolewa wakati huo. Amesema kauli ya Warioba kwamba idadi ya vifo iliyokuwa ikisemwa ingeifanya Tanzania kuwa na vifo vingi kuliko vilivyotokea katika Vita ya Kagera ilikuwa ni kutumia taarifa zisizothibitishwa katika kuto
Joseph Yona
Region: TZ
Friday 04 September 2026 11:46:08 GMT
Music
Download
Comments
user8315325576885kyambuko :
Lakini Hamwoni kama bara tunaliwa
2026-09-04 17:05:35
0
user5022410224176 :
Warioba alikuwa mmoja wa lile kundi la G55 akiwa amejificha nyuma ya pazia kwa sababu ya unafik. Alipo pewa uenyekiti wa tume ya katiba ndiyo akaikomalia hoja yake ya serekali 3.
2026-09-04 15:27:24
0
To see more videos from user @joseph_yona_, please go to the Tikwm
homepage.