@wizara_sanaatz: Teknolojia ya Kisasa ya Kufyatulia zege "Precast" imekuwa tumaini jipya katika kuongeza kasi ya ujenzi ya Uwanja wa mpira wa miguu Dodoma. Hayo yamesemwa Septemba 04, 2026 na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa wakati alipotembelea uwanja huo uliopo Kata ya Nzuguni, ili kujionea maendeleo ya mradi pamoja na vifaa vya "Precast" vilivyoletwa na mkandarasi hivi karibuni. Msigwa amesisitiza kuwa, matumizi ya teknolojia hiyo yanatarajiwa kuwa miongoni mwa hatua zitakazosaidia kuharakisha utekelezaji wa mradi huo na kuhakikisha ujenzi unaendelea kwa kasi iliyokusudiwa.