@jambotv_: VIDEO: Mkutano wa Kitaifa wa Wadau wa Kutafakari Hali ya Siasa nchini wa Septemba 8, 2026, umegeuka uwanja wa mnyukano mkali wa hoja baada ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanataaluma ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA), Profesa Elgidius Ichumbaki, kukishutumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuendeshwa na "dude" lisilojulikana, huku Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira, akijibu kwa kuwataka wasomi kuacha kulinganisha hoja zao na "mambo ya mitandao ya kijamii". Profesa Ichumbaki amefunguka kumweleza mzee Wasira pamoja na viongozi wengine wa CCM kuwa wameshindwa kutekeleza wajibu wao wa kikatiba, kisheria, na kijamii wa kuisimamia serikali ipasavyo. Profesa Ichumbaki amekwenda mbali zaidi na kuhoji kama kweli CCM inayo mamlaka kamili ya maamuzi nchini, akidai kuwa kuna nguvu nyingine ya siri inayoratibu mambo. Aidha, amegusia ahadi ya CCM ya kuanzisha mchakato wa Katiba Mpya ndani ya siku 100 za kwanza za uongozi wa Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, akidai kuwa wanachama wanaosimama kudai katiba hiyo, na wengine kutetea haki nyingine za wananchi wamekuwa ‘wakiadhibiwa’ na kufukuzwa uanachama wa CCM. Akimjibu Ichumbaki, Wasira, amepinga vikali madai kuwa watu wanaoongea kwa niaba ya wananchi wanashughulikiwa akisema, “Yeye anasema mtu akisema kwa niaba ya mambo wanayotaka wananchi anashughulikiwa. Sio kweli. Na wewe kwa kuwa ni msomi, na wasomi wana sifa moja kubwa ya kufanya utafiti. Utafiti ni sehemu muhimu ya usomi. Usipotafiti utasema chochote tu. Utakuwa kama mitandao ya kijamii ambayo haina control”. Wasira amekitetea chama chake akisema kuwa wanachama na viongozi wa CCM nao ni sehemu ya wananchi na sio malaika, hivyo nao wana haki na uwezo wa kutoa maoni yao huru.

Jambo TV
Jambo TV
Open In TikTok:
Region: TZ
Tuesday 08 September 2026 14:40:17 GMT
259762
16704
390
627

Music

Download

Comments

24medgard
~Eli :
kweli sometimes kipara ni busara wakuu
2026-09-08 16:35:56
141
user3852971019163
user3852971019163 :
kwel kabsa brother umeongea point sana Mungu akulinde
2026-09-08 15:33:39
437
flavykiwale3
flavykiwale7 :
zee la ovyo ili
2026-09-08 15:31:30
219
johnomarygift
God is a provider :
give the country to young people 🥰🥰🥰
2026-09-08 20:41:13
0
user1751706361096
The middle :
mzee mwema kabaki 1 tu tz
2026-09-08 17:41:25
105
mashirima8
Masiara :
Let's put Tanzania in God's hand.
2026-09-08 18:16:41
0
ndenge_nini12_36
Bamnyong'ode :
Ila Wasira has point, lets be honest
2026-09-08 16:35:49
32
salim.mpinga.26
SALIM MPINGA 26 :
Mungu ikikupendeza bc fanya na hiki najua kwako ni kidogo ila kwetu ni kikubwa..🥰🥰
2026-09-08 15:45:53
88
mussaramadhan472
NEWTON_JR :
very fact god bless you
2026-09-08 17:09:11
1
bin.issa.ktchen.d
bin issa ktchen dish :
kiufupi CCM hatuitaki🙌
2026-09-08 17:54:58
38
abdalahmsangi111
abdalahmsangi111 :
ukweli unauma aisee
2026-09-08 15:21:23
110
yustace1957
Treasure :
mhhhh short on target 🎯 irtakiwa apaa
2026-09-08 19:45:32
0
youngmado4
youngmado :
yani October 29 imeathiri mchakato wa katiba lakini haikuathiri ushindi wa 98%
2026-09-08 17:20:51
54
gracenasho6
Grace :
Ukweli usemwa🙏🙏🙏🙏🙏
2026-09-08 15:48:33
28
samsonkisigo
king sam :
wasira mhhh
2026-09-08 19:22:09
0
godfrey.gumie
Godfrey Gumie :
kaka umetisha umeongea ukwel
2026-09-08 15:32:26
140
user9786391085171
[email protected] :
Education is Talking
2026-09-08 17:48:06
0
mussakimaro297
Mussa :
mzee hajajibu swali
2026-09-08 15:43:23
46
rapaitotaikomollel
rapaitotaikomolle :
kaka hongera umepeleka ukweli
2026-09-08 16:35:58
36
halima00144
Halima kisuda :
Kaka uko vizuri Sana na ukweli unauma
2026-09-08 15:37:34
39
msafirimgavilenzi
Msafiri Mgavilenzi :
eeee munguu tenda jambo kwa huyuu mzeee ikikupendeza mungu baba
2026-09-08 15:58:13
54
alitodommy
alito d ommy💵🎧 :
mbon me cjamuelew huyu mzee
2026-09-08 16:54:09
17
goodluckyjs
Goodlucky JS :
Dua za watanzania😂😂🙌🏿
2026-09-08 16:41:23
12
user7453010382842
user CanRap :
Ukweli mchunguuu 😅
2026-09-08 15:58:02
13
markmagari
mark magari :
uo niukweli mtupu kaka
2026-09-08 15:39:43
19
To see more videos from user @jambotv_, please go to the Tikwm homepage.

Other Videos


About