@shebyranco: Video zinazosambaa mitandaoni zimeonyesha hali isiyo ya kawaida katika eneo la pwani ya Mar del Plata nchini Argentina, ambapo maji ya bahari yalionekana kupungua kwa kiasi kikubwa na kuacha sehemu kubwa ya sakafu ya bahari ikiwa wazi. Hali hiyo ilisababisha mshangao kwa wananchi na kuzua maswali kuhusu iwapo bahari ilikuwa “imetoweka”. Hata hivyo, taarifa zinaeleza kuwa bahari haikukauka wala kutoweka. Kupungua kwa maji kulitokana na mchanganyiko wa upepo mkali uliokuwa ukivuma kuelekea baharini, mabadiliko ya hali ya anga na mawimbi ya chini sana (extreme low tide), hali iliyosukuma maji mbali na ufukwe kwa muda. Kwa muda wa saa kadhaa, sehemu za sakafu ya bahari na miamba ambazo kwa kawaida hufunikwa na maji zilionekana wazi. Baadaye, maji yalirejea baada ya mabadiliko ya hali ya hewa na mzunguko #NewsUpdate #BreakingNews #togolay24update