@almecky_tz: Mwakilishi wa Jimbo la Kijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Zanzibar, @badriya_atai ameonyesha upande mwingine wa ubunifu na burudani baada ya kushiriki moja kwa moja zoezi la kukuna nazi katika Bonanza la Kijini Shangwe. Badria hakubaki kuwa mtazamaji, bali aliingia uwanjani na kushiriki zoezi hilo la asili pamoja na wananchi, hatua iliyozua shangwe na burudani katika bonanza hilo. Bonanza hilo limewakutanisha wananchi katika michezo na shughuli mbalimbali kwa lengo la kuimarisha mshikamano, kuchochea vipaji na kuhamasisha maendeleo miongoni mwa wananchi wa Kijini. #Zanzibar #Tanzania #Habari #Football #Trending