@wizara_sanaatz: Safari yake ya mchezo wa mpira wa miguu ilianzia katika Klabu ya Yanga Princess, kabla ya kuhamia Dux Logroño nchini Hispania, kisha Al-Nassr ya nchini Saudi Arabia, na sasa ameweka historia kwa kufika Washington Spirit ya Ligi ya Soka la Wanawake (NWSL) Marekani. Clara Luvanga mwenye umri wa miaka 21 ameandika historia hiyo kupitia usajili wa dau la dola Milioni 2.3 unaomfanya kuwa miongoni mwa wachezaji wa kike wenye thamani kubwa zaidi katika historia ya soka duniani.