@rfi_sw: Wakati maandamano ya upinzani yakipangwa kufanyika Jumanne hii mjini Kinshasa, tume ya Kitaifa ya Haki za Binadamu (CNDH) inatoa wito kwa mamlaka kuwalinda waandamanaji badala ya ukandamizaji. Pia inawasihi waandaaji na waandamanaji kujiepusha na vurugu. Maandamano hayo yanakuja wakati hapo jana Rais Félix Tshisekedi aliunda kamati iliopewa jukumu la kuandaa utekelezaji wa mazungumzo ya kisiasa ambayo yanapingwa vikali na vyama vikuu vya upinzani. Kamati hiyo itakuwa na jukumu la kuandaa mashauriano, kufafanua mahitaji ya mchakato huo, na kuandaa hadidu za marejeleo na muongozo wake. @billybilali anaangazia kwa kina....