@wepesitv: Bi. Felister Akonaay, mwenye umri wa miaka 60, anatarajiwa kufanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwezi Novemba mwaka huu katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu, akitoa somo kwamba elimu haina ukomo wa umri. Bi. Felister alihitimu elimu ya msingi mwaka 1982, lakini ndoto yake ya kuendelea na sekondari ilikatizwa na changamoto za kifamilia, ikiwemo kifo cha baba yake. Baada ya kuingia katika maisha ya ndoa, kupata watoto na wajukuu, hakuruhusu changamoto hizo kuifuta ndoto yake. Aliamua kurudi darasani na kuanza masomo ya sekondari, ambapo tayari amemaliza Kidato cha Kwanza na cha Pili na sasa anaendelea kujiandaa kwa mtihani wa Kidato cha Nne. Akieleza sababu ya kurejea shuleni, Bi. Felister amesema alikuwa na ndoto ya kwenda sekondari tangu utotoni, lakini hakupata nafasi kwa wakati huo, hivyo alipoipata fursa baadaye maishani akaamua kuitumia kutimiza ndoto yake. Amewataka vijana kutumia vizuri fursa za elimu walizonazo na kusoma kwa bidii ili kufikia ndoto na malengo yao. Walimu wake wamempongeza kwa juhudi, nidhamu na ujasiri aliouonyesha katika safari yake ya elimu, wakisema amekuwa mfano wa kuigwa kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla. Safari ya Bi. Felister inabeba ujumbe mzito: kuna ndoto zinaweza kuchelewa, lakini kuchelewa hakumaanishi zimekufa.
WEPESI TV
Region: TZ
Tuesday 15 September 2026 09:41:23 GMT
Music
Download
Comments
Theddy :
hongerena sanaaaa elimu Haina mwisho
2026-09-15 10:21:55
381
Dina kagina :
Amenpa nguv Na diploma yangu nisome degree Sasa. 😂😂
2026-09-15 11:52:40
46
shant❤️ :
😳😳😳unatK chet naww😭
2026-09-15 20:08:51
0
mom Richie😘🥰 :
ningekuwa rafk yake maana atakuwa anajua vitu 😂😂😂
2026-09-15 10:19:49
222
Elimido :
this teaches us to never give up
2026-09-15 18:50:01
1
Ney julius :
yaan mm Nina miaka 33 nashindwa nn Sasa kusoma??
2026-09-15 10:16:41
92
sasha :
Nachoka,kama cjaelewa.nina miaka 43 mbn kama nitaweza
2026-09-15 10:12:02
31
Angel bless :
Anasoma akiwa amestaafu tayari ila hongera🥰
2026-09-15 13:06:04
30
The Giant slayer🦕 :
umemzid Ex wangu alifeli form two 2021
2026-09-15 11:50:58
2
miss jp :
Basi sina haraka acha nitafute kwanza ada nitarudi
2026-09-15 14:45:25
19
user22949135569408 :
ndoto lazm zit im is
2026-09-15 11:39:59
2
N :
au mbingun kuna ajira nrud zangu shule
2026-09-15 10:46:23
12
Badface :
dah me nilikata tamaa kumbe bado safar ndefu aisee. ngoja nikaze
2026-09-15 11:51:48
14
Nafsa Hamis :
congratulations bibi
2026-09-15 16:35:10
0
lucy kidotii :
serikal inakutambua lakin mumy
2026-09-15 10:32:49
11
gagarinho_77 :
Ili aje awe naniii?
2026-09-15 11:59:51
6
Moana 🐚🌊🐬🦀🪷 :
samaani bibi ww ni mchaga au ?
2026-09-15 12:32:45
5
Elliana :
Akimaliza 4m4 tyr kashastaaf sasa itakuwaje ndg serikal 🤔
2026-09-15 12:01:50
10
mr- niko :
swez soma darasa moja na wazee mie
2026-09-15 10:15:48
12
p :
sasa mm. nan31 yangu nafeli wapi narudi shulee dadekkki daktiiimarto ya gen
2026-09-15 11:07:11
7
King Robinson :
Nipo Dar natafuta mdada tuchangie kodi tuake wote
2026-09-15 18:31:01
1
keyyl. :
mi Nina 28 na sithubutu kurudi shule
2026-09-15 15:47:16
3
Mishy 😻😻 :
Nipo dar natafuta mkaka tuchangie kod
2026-09-15 19:48:43
3
To see more videos from user @wepesitv, please go to the Tikwm
homepage.