@jambotv_: VIDEO: Katika kuendelea kwa maswali ya ufafanuzi ya Lissu kwa shahidi wake wa tano, John Heche, leo Septemba 16, 2026, Lissu amemtaka Heche afafanue majibu yake kuhusu ripoti za waangalizi na taasisi za kimataifa kama SADC na kueleza kile kilichosemwa mbele ya majaji kuhusu suala la utekaji. Heche amefafanua kwamba katika ukurasa wa 6 wa ripoti hiyo ya SADC, ulizungumzia masuala ya utekaji. Kutokana na Jibu hilo, Wakili wa Serikali Mkuu Nassor Katuga, alisimama na kupinga na kueleza kuwa hicho ni kipengele cha Re examination na siyo Examination in Chief, akidai kuwa Heche anaanza kusema mambo mapya. Tundu Lissu alijibu madai hayo ya Wakili wa Serikali Mkuu Nassor Katuga kuwa, kitu anachokubaliana na Wakili huyo ni kutajwa kwa ukurasa wa 6 pekee ambao awali shahidi hakuutaja, akisema mengine yote yaliyosemwa na shahidi yalikuwa sahihi. Lissu aliendelea kumuuliza Heche amwonyeshe kwenye ripoti ya SADC kuhusu utekaji pale aliposoma ili afafanue, na Heche alithibitisha kuwa ni kweli kwenye ripoti hiyo ya SADC ilizungumzia pia suala la utekaji.
Jambo TV
Region: TZ
Wednesday 16 September 2026 15:25:19 GMT
Music
Download
Comments
Merry Riziki :
hamna shida si watarudi tuu !!!
2026-09-17 12:13:08
0
Victoria GL :
wameenda masomoni watarudi 2032
2026-09-16 17:28:00
0
douglasalpho :
waongo leo nimeuona msafara wa IGP akirud hom jion hii
2026-09-16 18:28:43
1
SAMEER FASHION :
[Heartwarming]
2026-09-16 18:30:44
0
To see more videos from user @jambotv_, please go to the Tikwm
homepage.