@health_farm_tz: DR. LUKA MKENI anaeleza kuhusu uwepo wa kemikali zinazoweza kuzalishwa wakati wa upikaji na usindikaji wa nyama, ambazo zimehusishwa na ongezeko la hatari ya saratani, ikiwemo saratani ya utumbo mpana. Upikaji wa nyama kwa joto kali, hasa kuchoma, kuoka au kukaanga, unaweza kuzalisha kemikali kama Polycyclic Aromatic Hydrocarbons (PAHs) na Heterocyclic Amines (HCAs). Aidha, nyama zilizosindikwa kama sausage zinaweza kuwa na misombo ya N-nitroso, ikiwemo nitrosamines, ambayo imehusishwa na hatari ya saratani. Hivyo, aina ya nyama, kiasi kinacholiwa na namna inavyopikwa au kusindikwa ni mambo muhimu ya kuzingatia katika ulaji wa nyama. Aidha, Kumbuka kuwa kwa mujibu wa GLOBOCAN 2022, Saratani ya Utumbo mpana ni saratani inayoshika nafasi ya 5 katika orodha ya saratani zinazoongoza nchini Tanzania huku saratani ya Shingo ya kizazi ikiongoza kwa wanawake na saratani ya tezi dume ikiongoza kwa wanaume. ELIMIKA, HAMASIKA, CHUKUA HATUA KABLA MWILI HAUJACHOKA! CREDIT: wasafiMedia & Dr Luca Mkeni #healthfarmtz #nyama #saratani #tiktoktanzania #afya
health_farm_tz
Region: TZ
Thursday 17 September 2026 05:24:17 GMT
Music
Download
Comments
Salma :
wagonjwa watarajiwa wako weng Mwenyezi Mungu tusaidie
2026-09-17 15:44:46
2
user4921157175675 :
tuleni tu , bila nyama mambo yatakuwaje
2026-09-17 16:21:19
2
Rama Kazili :
Tulenini sana
2026-09-18 06:47:45
0
Omega :
duh
2026-09-17 19:32:06
0
Abuu Abdillah Assalafiyya :
🙏
2026-09-17 05:46:06
1
Majani Mabichi :
nisikilizeni mimi kuleni Nyama. Mboga mboga zina Madawa
2026-09-18 06:16:39
0
To see more videos from user @health_farm_tz, please go to the Tikwm
homepage.