@chawamata_tv: VIDEO: Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, SACP William Mkonda, amesema kabla ya kuanza utekelezaji wa Mfumo wa Pointi kwenye leseni za udereva, Jeshi la Polisi linatarajia kutoa elimu ya kutosha kwa madereva na wadau wa usalama barabarani. SACP Mkonda amesema hatua hiyo imechukuliwa baada ya kubaini kuwepo kwa mashaka na taarifa zinazozagaa katika makundi ya WhatsApp na maeneo mengine kuhusu mfumo huo, akisisitiza kuwa kanuni ipo tayari, lakini elimu inapaswa kutolewa kwanza kabla ya utekelezaji wake. Amesema katika zoezi hilo watatoa vipeperushi vyenye maelezo kuhusu namna mfumo huo utakavyofanya kazi, makosa yanayoweza kuhusishwa na pointi pamoja na mambo ambayo madereva wanapaswa kuyafahamu ili kujilinda dhidi ya ukiukaji wa sheria. Aidha, SACP Mkonda amekanusha taarifa kwamba kwa sasa madereva wanapopewa tiketi za makosa ya barabarani wanakatwa pointi kwenye leseni zao, akieleza kuwa alama zinazoonekana kwenye mfumo zilikuwepo tangu kipindi cha majaribio cha mwaka 2014 na hazimaanishi kuwa pointi mpya zimekatwa kwenye leseni za madereva. Amesema ili pointi ziweze kuhusishwa moja kwa moja na leseni ya dereva, mfumo huo unatakiwa kuunganishwa na mfumo wa mamlaka inayohusika na utoaji wa leseni. SACP Mkonda amewataka viongozi wa madereva na wadau wengine kuwa sehemu ya kutoa elimu badala ya kueneza taarifa zisizo sahihi, akisisitiza kuwa viongozi wanapaswa kuwa walimu na kusema ukweli kwa wanachama wao. Amesema lengo ni kuhakikisha elimu ya kutosha inatolewa na changamoto zilizobainishwa na viongozi wa madereva zinashughulikiwa kabla ya kuanza utekelezaji kamili wa mfumo huo. #ChawamataTV #10KFollowers #Asanteni #ChawamataTV #10KFollowers #Asanteni #ChawamataTV #10KFollowers #Asanteni #DarEsSalaam #Tanzania #Bongo #Habari #HabariLeo #BreakingNewsTZ #TanzaniaNews #BongoUpdates #TzUpdates #TzNews #BongoMedia #MediaTanzania #OnlineTV #trendingréels #tanzaniatrending #polisiviral #Asanteni #tanzaniatrending_habari #tanzaniatrendingsong #mediatanzania #tanzaniatrendingvideos #tanzaniatrendingstory #TanzaniaTre #madeintanzania🇹🇿 #madeintanzan #madeintanzania #SupportLocal #madeintanzaniat #roadto100followersontwitch #madeintanzaniawith #chawamata_tv #viraltz

CHAWAMATA TV
CHAWAMATA TV
Open In TikTok:
Region: TZ
Thursday 17 September 2026 07:28:11 GMT
85407
3239
243
628

Music

Download

Comments

akayohaog
akayoha og :
naona Kuna mpango wa kubadili gia angani
2026-09-17 08:13:27
57
t405dgb2
J4 :
Makosa ya gari mpeni mwenye gari yakwangu kiuendeshaji nipeni mimi
2026-09-17 08:18:21
31
user13697363833425
zuberi_mchilima13 :
point za nn kwani kuna ligi ya madeleva
2026-09-17 08:11:46
48
e.e.16689
E E 16689 :
ponti hata Kenya zipo ila sio makosa ya kuovatek au kutowasha ta, ponti inakatwa pale inapo tokea ajali kubwa ya kuua kwauzembe,
2026-09-17 08:28:22
27
kingmuubay
king muubay 24 :
chamsingi madereva hakuna kuingia rodi bhana
2026-09-17 11:11:18
3
lusekelonelson1
lusekelonelson1 :
oyooooooo line hiii
2026-09-17 09:46:04
0
ustadhwatanzania
USTADHI WA TANZANIA :
hizi point zimaisha tu, ina maana dereva yeye hashindi tuwe tunapata point
2026-09-17 10:32:47
4
lusekelocharles30
mmojawapo :
[Laugh approved][Laugh approved][Laugh approved] political
2026-09-17 07:42:42
0
jumaigoi
rj magar :
mbn me nimekatw
2026-09-17 08:54:57
0
kimoda90
Kimoda :
kwani hii nchi ikoje mbona wanatuona mashwain
2026-09-17 08:19:34
8
tamimuupdate
Tamimu Update :
toeni tu
2026-09-17 09:13:19
0
josephkamili.gwan
Jose Paroko :
29 tena
2026-09-17 10:19:32
0
richardjohanes591
Richie :
fungeni vifaa maalumu vya kurekodi makosa barabarani hii itasaidia sana
2026-09-17 08:32:14
7
hemedibarutingoma
Hemedi Baruti ngoma :
atutaki
2026-09-17 08:50:09
0
peterkulwa0
peterkulwa982 :
neno POINT hatutaki kulisikia kwenye Resen zetu
2026-09-17 10:43:41
2
fadymoses1
fadymoses 🚚 Truck driver ✔️ :
mpango waku felisha September 29
2026-09-17 09:31:34
3
kidogomazitocargo
Nelson Majaliwa :
me jana imeandikwa fain mbili zinaonyesha remain 13 point
2026-09-17 09:04:49
0
bagabriellamlt
👑 KiBELLa oG :
HAPA JESHI LA POLICE WANAKINZANA WENYEWE KWA WENYEWE SASA 🤔🤔🤔 RSA KULE WANAENDELEA NA KUTUKANDAMIZA KWA KUTUMIA CLIP ZA TRAFFIC WA KIGOMA KATIKA KITUO KIMOJA
2026-09-17 08:10:41
5
1stliboy
lastborn :
kama hazina madhara sasa ni za NN??
2026-09-17 09:02:45
1
mselasmarty
💥 𝗪𝗔𝗦𝗘𝗟𝗔 𝗦𝗠𝗔𝗥𝗧𝗬👣 :
Me jana kosa moja wamenikata points 6 zikabaki 9 kisa stika ya nenda kwa usalama na gari ni ya kampuni nilipiga hadi goti kuwaomba lakini haikusaidia
2026-09-17 13:51:29
1
seif.rashid2
Seif Rashid :
Alafu tuna bunge hii sheria ime tokea wapi ata hatujui
2026-09-17 08:37:11
0
jamse.mwangi
jamse mwangi :
Mbona tulikuwa tunapewa faini hakuna points
2026-09-17 08:30:40
4
charles.michael46
Charles Michael :
we mbona unauwa nyota haitolewe
2026-09-17 08:33:18
2
msingwa.jogging8
Ghost General trainer 🔥 🇹🇿 :
naona hapo ni mm tu sijaelewa kwenye maelezo hayo
2026-09-17 08:40:22
0
samdu039
SAMDU :
acheni kutuonea madereva .mnataka tufanye kazi gani.kwa nini madereva nchi hii
2026-09-17 09:29:34
4
To see more videos from user @chawamata_tv, please go to the Tikwm homepage.

Other Videos


About