@msumbanews: Mkuu wa Mkoa wa Geita, Alexander Mnyeti, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato kutoa gari lake aina ya Land Cruiser V8 na kulitumia kwa kubebea wagonjwa wanaohitaji rufaa katika Kituo cha Afya Muganza, baada ya gari la wagonjwa (ambulance) kuharibika matairi. Mnyeti ametoa agizo hilo wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi katika Soko la Kimataifa la Dagaa Kasenda, lililopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Chato, mkoani Geita, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kujitambulisha kwa wananchi.\ Akizungumza katika mkutano huo, Mbunge wa Jimbo la Chato Kaskazini, Cornel Magembe, amemuomba Mkuu wa Mkoa kuhakikisha ambulance ya Kituo cha Afya Muganza inapatiwa matairi mapya ili kurejesha huduma ya usafirishaji wa wagonjwa, hususan wanaohitaji kupewa rufaa kwenda hospitali. Kabla ya kuanza ziara yake ya kujitambulisha kwa wananchi wa Mkoa wa Geita, Mnyeti alianza kwa kutembelea kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, lililopo Chato. Baada ya hapo, Mkuu huyo wa Mkoa alikutana na baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato na kuwataka kutekeleza majukumu yao kwa bidii, huku wakizingatia kusikiliza na kutatua kero za wananchi kwa wakati. Mnyeti amesema viongozi na watumishi wa Serikali wanapaswa kuelekeza nguvu zao katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na changamoto zao zinatatuliwa kwa ufanisi.

Msumba News Blog
Msumba News Blog
Open In TikTok:
Region: TZ
Thursday 17 September 2026 09:16:30 GMT
51333
1768
91
117

Music

Download

Comments

_victory_vault
_zede1 :
This country is full of drama NGL🙌
2026-09-17 10:16:41
0
saba1725
Saba :
Maigizo, ambulance ni gari maalum kwa ajili ya kubebea wagonjwa. Hilo v8 halina vifaa maalum kwa kuweza kubeba wagonjwa. Na tunashangilia.
2026-09-17 10:33:13
10
eastherchristopher
Easther Christopher🥰❤️ :
kunawatu humu wanabisha ni kwa sababu shida ni ambulance na wanaotumia ni wagonjwa ndio maana wanaona kama DED kaonewa ila mkae mkijua hata kama sio ambulance ni V8 lakin itafikisha mgonjwa kwa wakati sehemu husika ya matibabu.... KWAHIYO WAGONJWA WAFE KISA V8 SIO GARI YA WAGONJWA?
2026-09-17 11:22:52
4
mainstein1
Alen :
ambulance ni gari na vifaa tiba vilivyo ndani ya gari hilo
2026-09-17 11:03:43
9
user3978724327287
TANZANITE :
lengo ni kwamba matairi ya ambulance yanapatikane haraka
2026-09-17 12:23:51
7
medyclassic745
Medy Classic745 :
sasa iyo gari ina quality ya kuwa Ambulance? au siasa tu
2026-09-17 10:25:55
6
larry.tee939
Larry 🎧💰 :
Et matairi hayapo tusubili ilaaaaa TZ yangu 😂😂😂
2026-09-17 10:24:53
1
geraldjabu1.com
Gerald Jabu1 :
Kwanini asinge agiza matairi ya humo yafunguliwe yafungwe kwenye ambulance 🚑 hiyo v8 haijatengenezwa kukidhi haja ya kubeba wagonjwa
2026-09-17 10:40:48
0
sayukisheshushi27
Sayuki Sheshushi :
huyu anataka sifa kwani akitoa matairi ya hiyo gari yake akaweka kwenye Ambulance shida ipo wapi mpaka atumie gari lisilo na huduma
2026-09-17 11:14:12
0
carrasco.nation32
Carrasco Nation :
Mi nshukur siku hiz watanzania tunajua kuchambua uhalisia wa vitu 😂😂
2026-09-17 10:26:50
3
addy.....1
Addy01 :
ambulance ni zaidi ya gari. c kila gari inatosha kua ambulance. hapa issue ya ambulance ikifatiliwa vzr inaweza kuibua mengi katika mnyororo wa huduma. lkn tukiamua tu kuzima mambo kirahic hivo, tutarajie lawama kila cku
2026-09-17 10:42:41
1
sosssossy2
Sossy :
mkuu wa mkoa kakulupuka
2026-09-17 10:45:32
0
nickokama
Nick Moshi :
safi kabisa
2026-09-17 13:52:50
1
drleon008
Drleon008 :
😂😂😂 jamani
2026-09-17 11:22:37
2
iamidrisor
🆔risor2️⃣5️⃣5️⃣ :
Siasa t hizo Hilo gar kesho t lipo mtaan na mkurugenz kama kawaida dah Asa v8 inakuaje ambulance hata sifa na kitanda cha mgonjwa kitakaaje
2026-09-17 11:11:41
0
corzone6
coràzone :
nilosema mkuu wa mkoa mpya n baraaa any way mbunge wetu mbona unatuzalilisha huku kwetu hii kesi hata dowan angejitolea kununia kwa pesa yake
2026-09-17 11:27:18
1
oliversteven376
oliversteven376 :
Dramaaaa
2026-09-17 13:13:25
0
ohymes264
One🏹 :
apo jion ana rudishiwa v8 yake ana peleka matairi
2026-09-17 12:54:12
0
bata.point.pub
BATA POINT PUB :
ila mnyeti bwana dah
2026-09-17 12:12:47
0
balaka.zacharia
Balaka Zacharia :
tungepata viongoz kama hawa 100 tu nchi ingeelewa. maana kunamkuu mja alishawahi kutamuka choo cha soko kitumike choo chakiongozi wakati anafanya mchakato
2026-09-17 11:38:49
0
mguu_wa_kutoka2026
MGUUWAKUTOKA :
mnashangilia kwa sababu hamjui kuwa selikali ina mifumo ya decentralization, kila kituo cha cha kutolea huduma kinajitegemea kwa kujiendesha, ni pesa chache ambazo hupangwa ndio hutumika. mkurugenzi anahusika tu kwasababu halmashauri nzima ni yake ... ila trust me hicho kituo watanunua mataili kwa pesa zao wenyewe, iwe kwa mkopo ama ama kwa cash
2026-09-17 17:27:37
0
jacksonlukuba
CALL ME HONEYBADGE! :
kuna jambo lifuatiliwe nani ni shida hapo
2026-09-17 12:37:47
0
mrtanapa
[email protected] :
yanafungwa siku hyo hyo mkurugenzi ma v8
2026-09-17 15:19:02
0
manuuel000
senya :
@senya:pia hapo ambulance yenyewe kumbuka kibongo bongo ni landcruiser 1Hz, haina umaalumu mkubwa ambao hiyo V8 itashindwa kwa kitambo kidogo
2026-09-17 13:15:31
0
inkwale8
inkwale :
hapo safi sana
2026-09-17 10:17:32
0
To see more videos from user @msumbanews, please go to the Tikwm homepage.

Other Videos


About