@gerry__patrick: Moja kati ya video inayo'trend sana kwenye mitandao ya kijamii ni hii inayomwonyesha Mwamuzi (Referee) Ramadhan Kayoko akifanya mazoezi ya utimamu wa mwili kwa njia ya karate Ishara hiyo inaweza kuzua umakini kuelekea dabi ya kariakoo kati ya @simbasctanzania na @yangasc huku tukikumbuka jopo la waamuzi kuelekea mtanange huo bado halijawekwa wazi Je, kama Ramadhan Kayoko atapewa jukumu la kuwa pilato wa Mchezo huo, Unadhani timu gani itapata wakati mgumu kwenye maamuzi ya mwamuzi Kayoko?